“TUMIENI MVUA HIZI KWA KILIMO”RC KUNENGE.

Na Shushu Joel.Mkuranga.

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amewataka wakulima wote walio kwenye Mkoa huo kuhakikisha wanatumia fursa ya mvua zinzoendelea kunyesha sasa kwa kulima mazao yanayostahimili ukame

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akifikilia jambo (NA SHUSHU JOEL)

Akizungumza kwenye kikoa kazi Rc Kunenge alisema kuwa kipindi hiki Mungu ametushushia neema ya mvua hivyo ni vyema tukatumia nafasi hiyo kulima mazao ya haraka kwa ajili ya chakula cha familia.

“Ni vyema tukatumia mvua zinazoendelea kunyesha sasa kupanda mazao yatakayoweza kuvunika haraka ili tupate chakula kwa mahitaji ya familia zetu”Alisema Kunenge

Aidha alisema kuwa ni vyema wataalamu wetu wa Ugani mkatumia kipindi hiki ambacho mvua zinaendelea kunyesha kwenye Mkoa wetu kwenda moja kwa moja kwa wakulima wetu kuwapatia elimu ya kutosha juu ya kulima mazao ya muda mfupi na yenye tija kwa wananchi.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Mkuranga Bi, Khadija Ally amemshukuru Mkuu wa Mkoa Kunenge kwa maono yake ya mbali kwa wananchi wa wilaya hiyo na Mkoa kwa ujumla.

Aliongeza kuwa wilaya ya Mkuranga imekwisha weka mikakati ya kutumia mvua hizi zinazoendelea kunyesha kwa kuwafuata wakulima na kuwapatia elimu juu ya kuchangamkia fursa za mvua hizo kulima mazao sitahiki na yenye kukomaa haraka.

“Kwa kweli Mkuu wa Mkoa Mhe: Kunenge amekuwa msaada mkubwa kwetu kwani amekuwa akitushauri mambo mengi kwa kusudi la ufanikishaji wa mahitaji ya wananchi yaweze kufurahianserikali yao chini ya awamu ya sita” Alisema Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga.

Naye Mmoja wa wakulima wa wilaya ya Mkuranga Ngd Mwarami Juma mara baada ya kufanya mahojiano na HABARI MPYA BLOG alisema kuwa tunampongeza Mkuu wa Mkoa kwa jinsi ambavyo amekuwa na jicho la tatu kwa wananchi wake wa Mkoa wa Pwani na hasa katika kuwapambania kuweza kufikia malengo ya maisha mazuri kwa kutuymia Raslimali zetu.

Aliongeza kuwa elimu ambayo amekuwa akiitoa kwa wananchi wa Pwani ni wazi kabisa kiongozi huyu anatamani kumuona kila mwananchi wa Pwani ananufaika na Mkoa huo.

Aidha amewashauri wakulima wenzake kutumia nafasi za mvua hizi kupanda mazao stahiki na yenye kukomaa haraka ili kuweza kupata mavuna mengi kwa muda mfupi na ndio maana Mkuu wa Mkoa ametushauri tutumie mvua hizo kujinufaisha kwa kilimo.

MWISHO

 

Post a Comment

0 Comments