Na Shushu Joel,Kibiti.
MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge kwa niaba ya wananchi wa kibiti amempongeza Mhe: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha ujenzi wa daraja la Mbushi Mwera jambalo ambalo wananchi wa maeneo hayo walikuwa kama wapo kifungoni kwa kipindi cha muda mrefu sasa.
![]() |
Waziri Mkuu Kssim Majaliwa akisikiliza maelezo ya ujenzi wa daraja hilo(SHUSHU JOEL) |
Kauli hiyo ameitoa alipokuwa
kwenye ziara Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipotembelea taraja hilo ili kujionea
namna gani Rais Samia amemaliza changamoto hiyo ilikuwepo tangu tupate uhuru.
“Tulikuwa na Changamoto kubwa
ya Daraja hapa Mhe Rais ameleta fedha na Daraja hili linejengwa. Eneo hii
ilikuwa haliipitki” Alisema Kunenge
Aidha Kunenge ameeleza kuwa eneo hili la Mbuchi ni
eneo la Kimkakati kwa Uchumi wa Mkoa kwani kuna shughuli kubwa za Kilimo na
Uvuvi zinzzofanywa na wananchi kwa ajili ya kujiongezea kipata na uchangiaji wa
pato la serikali kwa ulipata wa kodi mbalimbali
Mhe: Rais amefanya kazi kubwa hana ubaguzi anatuhudumia na kupeleka huduka kule kwenye Changamoto zaidi.
Waziri Mkuu wakionyeshana kitu na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge(NA SHUSHU JOEL)
“Wilaya za Kibiti na Rufiji
shughuli kubwa zinzofanya ni Kilimo cha korosho, Mpunga Ufuta. "Tuna Uwekezaji
Mkubwa kilimo cha Mpunga Wilaya ya Kibiti" Alisema Rc Kunenge
Hata hivyo kumekuwa na wimbi
kubwa la Wawekezaji kukimbilia eneo hili kwa sababu lina Maji na Ardhi nzuri
yenye rutuba
Pia Kunenge ameeleza kuwa Kutokana na Changamoto ya Mabadiliko ya Tabia
Nchi Wafugaji Wengi wamehamia Wilaya ya Rufiji na Kibiti, hali inayopelekea
Mifugo kuwa mingi kuliko ukubwa wa Ardhi iliyotengwa kwa malisho.
Mhe Kunenge ameeleza Mkoa
Unaendelea na kutoa elimu kwa Wakulima kufuga Mifugo kulingana na Ardhi ya
Malisho. Ameeleza Mkoa unatekelezwa Mpango wa Ranchi Ndogo na wameanza kwa
Wilaya ya kisarawe tuna Ufugaji na kibiti tuna Ufugaji wa Ranchi Ndogo.
Kwa upande wake Waziri Mkuu
Kassim Majaliwa ameridhishwa na Ujenzi
wa Dajara Hilo amepongeza Taasisi za TANROADS na TARURA kwa kazi nzuri ya
Usimamizi na Ujenzi wa Daraja hilo.
Ameeleza kuwa Ujenzi wa Daraja
hilo ni dhamira ya Serikali ya Kuhakisha inawafikia Wanchi mpaka Vijijini Hivyo
ndiyo maana Serikali imeanzisha Wakala wa Serikali wa Barabara Vijijini TARURA
ili kumaliza changamoto za barabara kwa wananchi .
Aidha Waziri Mkuu amemwagiza
Waziri TAMISEMI Kushughulikia Ujenzi wa Barabara Unganishi kutokea Mhoro
kufika Mbuchi.
Pia amewataka Wananchi
kuchangamkia Fursa za Kiuchumi zilizopo katika eneo hilo ili kuweza kujipatia
kipato kitachonufaisha familia zao
Katika Hatua Nyingine Mhe
Majaliwa amewataka Wafugaji kufuga kulingana na Maeneo wanayoyamiliki.
Ameelekeza Serikali za Vijiji zitambue Mifugo yote iliyopo na Maeneo yao na
Viongozi ngazi ya Mkoa na Wilaya kusimamia kila Mfugaji awe na eneo la kufugia.
Aidha Waziri Mkuu Majaliwa amekemea Tabia ya mapigano ya Wakulima na
Wafugaji na kutaka wachukuliwe hatua kwa mfugaji ambaye hathamini maisha ya
wengine.Aidha Mhe Majaliwa ameitaka Halmashauri hiyo kujenga Zahanati kila
kijiji kupitia fedha za ndani.
Amesisitiza Utunzaji wa Misitu
ya Mikoko na kutaka Wananchi wa Mbuchi kutafuta chanzo kingine cha mapato na
Biashara kwa Ukataji wa Miti huo utathiri Mazingira na vyanzo vya Maji.
MWISHO
0 Comments