MUSSA MANSOUR AWAFUTA MACHOZI WALEMAVU.

Na Shushu Kibaha.

MJUMBE wa kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani Mussa Mansour amefanikiwa kukutana na kundi maalum la watu wenye ulemavu katika wilaya ya Kibaha Mkoa Pwani na kuwasaidia mahitaji mbalimbali.

Mjumbe wa halmashauri kuu na kamati ya siasa Mkoa wa Pwani Mussa Mansour akimpatia sadaka mtoto mwenye ulemavu (NA SHUSHU JOEL)

Akizungumza na walemavu hao waliojitokeza kwa wingi katika ofisi zao zilizoko maeneo ya kwa Mfipa kata ya Kibaha Mansour alisema kuwa kutoa ni moyo na sio utajiri, pia tumeambiwa na mwenyezi Mungu kuwa tuwakumbuke kwa chochote wenzetu wasiojiweza na hasa katika kipindi hiki cha mfungo wa  mwezi wa Ramadhani.

“Ndugu zangu nawathamini sana ndio maana leo nimekuja kuwapatia futari hii ndogo ili nanyi mkaweza kula na familia zenu ingawa nilitamani nipite kwenye majumba yenu ili niwagawie huko naombeni mnisamee sana kwa hilo” Alisema Mansour

Aidha Mjumbe huyo wa kamati ya siasa ya CCM Mkoa wa Pwani amewakumbusha wananchi wenye nafasi hapa duniani kujitoa kwa wale wenye uhitaji ili kuweza kupata baraka kutoka kwa Mwenyezi Mungu wetu pale tunapowasaidia watu wenye mahitaji.

Baadhi ya walemavu waliojitokeza kupokea sadaka kutoka kwa Mussa Mansour 

Aidha Masour amewalipitia madeni yote waliyokuwa wakidaiwa walemavu hao katika ofisi yao ikiwemo maji na kuwanunulia matofali elfu moja  kwa ajili ya ujenzi wa ofisi yao na kuwapatia kiasi cha shilingi milioni mbili zitakazowasaidia katika ofisi yao

Katika zoezi hilo Masour aliongozana na sheikh wa Mkoa wa Pwani Hamis Mtupa ambapo amempongeza sana kwa jinsi ambavyo amekuwa akijitoa kwa jamii.

Aidha Sheikh Mtupa amemtaka Mansour kuendelea na moyo huo wa kujitoa kwa jamii na hasa watu wasiojiweza kwani anachokifanya sasa ni baraka kubwa kesho .

“Mwenyezi Mungu anamakusudi makubwa juu yetu kutokana na kwanini mimi ni mzima wa viungo na wewe ni mlemavu hivyo tuendelee kuwasaidia wenye uhitaji” Alisema Sheikh wa Mkoa wa Pwani Mtupa

Kwa upande wake katibu wa walemavu Mkoa wa Pwani Mwalimu Bundara amempongeza Masour kwa kuwafuta machozi ambayo yalikuwa yakiwatiririka bila kujua nani ni mkombozi wao.


Aidha amemtaka aendelee na moyo huo na wao watazidi kumuombea kwa Mwenyezi  Mungu ambariki na kumjalia kila hitaji la moyo wake

“Leo walemavu mbalimbali tumepokea misaada mingi ikiwemo futari ya siku tatu na fedha hii yote ni neema kubwa kwetu kwani tulikuwa hatujui nani atajitokeza kutusaidia lakini kumbe Mwenyezi Mungu anamleta Masour Asante sana kwa niaba ya walemavu” Alisema Mwalimu Bundara.

MWISHO

Post a Comment

0 Comments