Na Shushu Joel,Bukombe
MWENYEKITI
wa Jumuiya ya Wazazi (CCM) wilaya ya Bukombe Mkoani Geita Hassan Abdalah
amesema kuwa Jumuiya hiyo ni chachu ya maendeleo na malezi bora kwa watoto hapa
Nchini.
Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo alipokuwa akizungumza na wana Chama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kata ya Bulangwa
Mwenyekiti wa Wazazi wilaya ya Bukombe Ndugu Hassan Abdalah akisema neno kwenye Mkutano huo (NA SHUSHU JOEL)
Alisema kuwa
Jumuiya hii ni nguzo kubwa katika mambo
mengi hivyo kila kiongozi aliye ndani ya jumuiya yetu ni muhimu kuweza
kujitafakali kwa kina juu ya uwezo wake wa kuongoza na kusaidia jamii yetu
katika Nyanja mbalimbali za kimaendeleo
Aidha
amewataka viongozi wa jumuiya hiyo kuendelea kuyasema yale mazuri yanayofanywa
na Rais wetu wa jamhuri ya Muungno wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwani
maendeleo anayoyafanya yamezidi kuwa msaada mkubwa kwa wananchi waTanzania.
“ Sasa hivi
kuna mashule, zahanati, vituo vya Afya , miundombinu bora ,umeme, maji na
mengine mengi ambayo Rais wetu amekuwa akiyafanya” Alisema Hassan ’
Naye katibu
wa ccm wa kata hiyo Edmond Bagelezi alisema kuwa Mwenyekiti wa wazazi wilaya ya
Bukombe ametuachia deni kubwa wana ccm hivyo tuna mwakikishia tutafanya kazi
kwa bidii ili kuhakikisha ccm inazidi kuwa juu kama ilivyo sasa.
Aidha
amewataka viongozi kuyafanyia kazi maneno yaliyosemwa na mwenyekiti wa Wazazi
ili kuweza kuongeza ufanisi wa utendaji kazi.
Pia katibu
huyo amempongeza mbunge wa Jimbo hilo ambaye pia ni Waziri wa Nishati na Naibu
Waziri Mkuu Dkt Dotto Biteko kwa jinsi ambavyo amekuwa msaada mkubwa katika
ufanisi wa ufanikishaji wa maendeleo katika kata hiyo kwani awali kata hiyo
ilikuwa nyuma sana lakini sasa hivi tunaweza kusema kuwa Mhe Biteko ni mfano wa kuigwa.
MWISHO
0 Comments