MKUU wa wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani Philberto Sanga amewatumbua viongozi watatu wa kijiji cha Kibesa kata ya Kisegese wilaya humo kwa tuhuma za matumizi mabaya ya ofisi dhidi ya wananchi.
Mkuu wa wilaya ya Mkuranga Philberto Sanga akisisita jambo mbele ya wananchi wa kijiji cha Kibesa(PICHA NA SHUSHU JOEL) |
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha kibesa wakimfuatilia mkuu wa wilaya ya Mkuranga Philberto Sanga hayupo pichani (PICHA NA SHUSHU JOEL) |
Aliongeza kuwa anawapongeza wananchi kwa ujasili wao wa kusema ukweli kwa maovu wanayofanyiwa na viongozi hao wasiokuwa na maadili
Mtendaji wa kijiji hicho Bw,Ally Hamis aliyesimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi(SHUSHU JOEL) |
Pia Mkuu huyo wa wilaya amemwagiza mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kibesa kuilipa mifuko ya saruji zaidi ya 40 iliyotolewa na serikali kwa ajili ya kuweka sakafi kwenye darasa na matokeo yake ikaganda na kupelekea kushindwa kutumika.
Mkuu wa wilaya akipokea malalamiko ya wananchi yaliyowasilishwa na mtendaji wa kata |
Kwa upande wake Samwel Kimose alimpongeza mkuu huyo wa wilaya kwa kutambua thamani ya wananchi wa kijiji cha Kibesa kwani walikuwa wakiteseka kwa kipindi kirefu kwa viongozi hao kujiona ni Mungu watu.
Aidha amemkabidhi mkuu huyo wa wilaya nyaraka mbalimbali ambazo zilikuwa zikitumiwa na viongozi hao kwa kuuza maeneo mbalimbali ya kijiji huku wakitoa risiti feki.
Mmoja wa wakazi wa kijiji hicho ambaye pia ni mwalimu wa shule iliyopo kijiji hapo akichangia hoja kwa mkuu wa wilaya.(SHUSHU JOEL) |
Aliongeza kuwa umoja,ushirikiano ndio utakao tuvusha kutoka hapa tulipo na kwenda mbele kimaendeleo
Wananchi wakiwa makini kumsikiliza mkuu wa wilaya Sanga(SHUSHU JOEL) |
MWISHO
0 Comments