KIKWETE ASHINDA KURA ZA MAONI

Na shushu joel

ALIYEKUWA mbunge wa jimbo la Chalinze Mh Ridhiwani Kikwete amefanikiwa kutetea nafasi yake ndani ya chama cha mapinduzi(CCM) kwa Kushinda washindani wake katika  kura za Maoni kuelekea uchaguzi Mkuu wa Uraisi, Wabunge na Madiwani uliofanyika katika viwanja vya msata mapema tarehe 20 Mwezi huu.

Mh Ridhiwani Kikwete akizungumza neno mbele ya wana CCM wenzake kabla ya kushinda kura za maoni.(NA SHUSHU JOEL)





Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi huo msimamizi  wa uchaguzi huo Msimamizi mkuu wa Uchaguzi huo Gullamu Kifu ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya kibiti alisema kuwa uchaguzi umekuwa ni wa wazi kama chama chetu kinavyotaka.

Aliongeza kuwa uchaguzi ulikuwa ni mkali lakini Kikwete ameibuka na mshindi wa kura 369 na kuacha wapinzani wake kwa kura zaidi ya Mia  moja.

Baadhi ya wajumbe wakifuatilia uchaguzi wa jimbo la chalinze(NA SHUSHU JOEL)
"Nimeamini Kikwete ni kipenzi cha wanachalinze kwani nimejionea mwenyewe kwa jinsi alivyoangusha wapinzani wake"Alisema Kifu. ' la Msingi kwao ni utulivu sasa maana kuna vikao mbele vitakavyoamua hatima ya mgombea wa jimbo hili.'

Aidha alisema kuwa waliokuwa wakimfuata kwa karibu ni Mwenyekiti wa ccm mkoa wa Pwani Ramadhani Maneno aliyepata kura 273,Said Zikatimu ambaye alikuwa ni Mwenyekiti wa halmashauri ya Chalinze kwa kupata kura 223,Imani Madega 33 na wagombea wengine 21 wakigawana kura zilizobaki.

Mh Ridhiwani Kikwete akipiga kura kabla ya kutangazwa mshindi wa uchaguzi huo.(SHUSHU JOEL)
Alisema kuwa jumla ya wagombea waliojitokeza katika kiwania nafasi ya ubunge jimbo la Chalinze walikuwa 26 ingawa mgombea mmoja alijitoa na hivyo kupelekea wagombea kubakia 25 huku wakinamama wakiwa 5. Ilikuwa ni uchaguzi wa Demokrasia ya Wazi sana. Pia amewapongeza wajumbe wote wa mkutano mkuu wa jimbo kwa utulivu waliouonyesha katika mkutano kuanzia mwanzo mpaka mwisho wa uchaguzi huo na Ridhiwani Kikwete kuibuka mshindi.

Naye mmoja wa wapiga kura kutoka kata ya kibindu Amina Juma(46) alisema kuwa uchaguzi umesimamiwa vizuri na wasimamizi walioteuliwa na chama hivyo Kikwete alikuwa ni chaguo la wanachalinze tu.

Mh Ridhiwani Kikwete akisaini mara baada ya kutangazwa mshindi.(SHUSHU JOEL)
"Nawaomba wana ccm wenzangu kuungano pamoja ili kuhakikisha uchaguzi mkuu chama kinapata ushindi wa kishindo hasa baada ya Chama kuteuwa Mgombea Mmoja"Alisema.Bi Amina.

Naye mshindi wa uchaguzi huo Mh Ridhiwani Kikwete ambaye hakutaka kuongea mengi alisema kuwa ushindi uliopatikana ni ishara tosha kuwa wanachama wa CCM wa Jimbo hilo bado wanamuhitajika kuendelea kuwatumikia hivyo amejipanga kutumika kwa maendeleo yao. "....... Kwa ushindi huu wa kura za maoni ni mwanzo tu hivyo tuendelee kumuomba Mungu ili jina liweze kurudi kutoka vikao vya ccm "Alisema.


Baadhi ya wana CCM wakicheza nyimbo za chama hicho kabla ya uchaguzi kufanyika.(SHUSHU JOEL)
Aliongeza kuwa naamini kwa kishindo hiki kura za Mh Rais Dkt John Pombe Magufuli kutoka jimbo la Chalinze zitakuwa ni zaidi ya 100% kutokana na yale yalitendeka katika jimbo la Chalinze. Hivyo amewataka wana ccm kuvunja makundi kwani uchaguzi umekwisha kwani ccm ni moja hivyo tupige kazi za maendeleo kwa jamii yetu.


MWISHO

Post a Comment

0 Comments