MSIMAMIZI wa kinyang'anyilo cha kuwania uwakilishi wa nafasi ya ubunge kupitia jumuiya ya vijana(UVCCM) Mkoa wa Pwani Omary Mtuwa amewatoa hofu vijana waliojitokeza kwenye ulingo huo.
| Msimamizi wa uchaguzi wa ubunge kupitia umoja wa vijana(UVCCM) mkoa wa Pwani ambaye pia ni katibu wa CCM wilaya ya Rufiji Omary Mtuwa akifafanua jambo (NA SHUSHU JOEL) |
"Wagombea wengi wamekuwa na imani kuwa yule anayeongoza kwa kura nyingi ndiye mshindi,hapana chama chetu cha mapinduzi kina utaratibu wa vikao mara baada ya kupeleka majina hivyo vikao ndivyo venye mamlaka juu ya nani anatakiwa kurudi ili kupeperusha bendera ya vijana"Alisema Mtuwa.
![]() |
| Omary Mtuwa msimamizi wa uchaguzi Uvccm mkoa wa Pwani akiwa na Khadija Ismail kulia mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi na Khadija kuongoza kura.(PICHA NA SHUSHU JOEL) |
"Chama cha mapinduzi (CCM) kinawategemea kwenye kufanya kampeni mara baada ya kutangazwa kuanza kwa uchaguzi mkuu kwa kutumia sifa zenu huko makwenu ili tuweze kupata ushindi wa kishindo kwenye nafasi za Madiwani,Wabunge na Rais"Alisema Mtuwa.
![]() |
| Baadhi ya wagombea wa nafasi ya uwakilishi wa ubunge kupitia jumuiya ya vijana (UVCCM) Mkoa wa Pwani(SHUSHU JOEL) |
Akisoma matokea mara baada ya kutoa angalizo la kutokusherekea James alisema kuwa Khadija Ismail amepata kura 15,Mary Joseph kura 8,Mufandii Msaghaa kura 6 na wa nne ni Cstherine Shayo aliyepata kura 2 huku wengine wakiambulia 1 na wengine 0 .
![]() |
| Khadija Ismail aliyefanikiwa kuongoza kura katika uwakilishi wa ubunge kupitia UVCCM mkoa wa Pwani kabla ya kupata matokeo(NA SHUSHU JOEL) |
![]() |
| Moja wa wajumbe wakipiga kura kwenye uchaguzi huo |
![]() |
| Msimamizi wa uchaguzi wa UVCCM mkoa wa Pwani kwenye uwakilishi wa nafasi ya ubunge akimkabidhi Mwenyekiti wa jumuiya hiyo karatasi ya kupigia kura.(NA SHUSHU JOEL) |
MWISHO





0 Comments