Na Shushu
Joel
MKURUGENZI
wa mtandao wa jinsia nchini (TGNP)Bi,Lilian Liundi ameungana na watanzania wote
nchini kuomboleza kifo cha aliyekuwa Rais wa awamu ya tatu Hayati Benjamini
William Mkapa huku akielekeza kuwa Taifa limepoteza nguzo ambayo ilikuwa mstari
wa mbele kwenye masuala ya kuweka usawa wa kijinsia nchini Tanzania.
![]() |
Mkurugenzi wa TGNP Lilian Liundi akifafanua jambo. |
Akizungumza
wakati wa kutoa salamu za rambirambi mkurugenzi huyo alisema kuwa katika
kipindi cha utawala cha Hayati Mkapa aliweka misingi mikubwa kwa ajili
kuendeleza usawa wa kijinsia katika nchi ya Tanzania na kisera,kisheria na
kitaasisi pia aliruhusu ushiriki wa makundi mbalimbali katika kufikia misingi
ya kijinsia.
“Nakumbuka
kipindi wanawake wanarudi kutoka Beijing kitu alichokifanya Mkapa ni kitendo
cha kuwapokea wanawake ingawa ndani yao hao wanawake baadhi waliambiwa waishie
uwanja wa ndege na ajenda yao ya Beijing lakini Hayati Mkapa aliwapokea
wanawake wote waliokuwa wameongozana na Balozi Getrude Mongella”Alisema Liundi
Aliongeza
kuwa katika upande wa Azimio la jinsia na maendeleo ukanda wa SADC Hayati Mkapa alikuwa mstari wa mbele
sana katika nchi za SADC, Tanzania zilikuwa moja wapo wa nchi zilizoshiriki kwa
kusaini Azimio hilo kwenye kipindi cha uongozi wake na kufikia kwa asilimia 30.
![]() |
Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Hayati Benjamini William Mkapa |
Aidha
aliongeza kuwa katika ngazi ya Afrika,Maputo protocal pia ilikuwa ni kipindi
cha Hayati Mkapa ambapo aliridhia mkataba kwa makusudi ya kuendeleza usawa wa
kijinsia huku akisema kuwa japo kuna mapungufu lakini kwa kipindi changu lazima
utekelezji uwekewe misingi imara zaidi.
Hivyo Liundi
alisema kuwa Hayati Mkapa atakumbukwa kwa mambo mengi aliyoyaanzisha hapa
nchini na kwa hali hii ni lazima kila mtanzania akimkumbuka machozi lazima
yamtoke.
MWISHO
0 Comments