SAGINI AKILI NANENANE SIMIYU IMEBAMBA.

Na Shusghu Joel,Simiyu.
 
ALIYEKUWA katibu Tawala mkoa wa Simiyu Jumanne Sagini amekili kuwa maonyesho ya Nane Nane mwaka huu ya  kanda ya ziwa mashariki yanayofanyika mkoani Simiyu yamekuwa na vivutio vingi kwa wakulima wa mkoa huo
Jumanne Sagini akiangalia njia ya kisasa ya uhifadhi wa nyuki kutoka kwenye Banda la mkoa wa Mara.(PICHA NA SHUSHU JOEL)





Akizungumza wakati alipokuwa akizunguka zunguka  kwenye mabanda mbalimbali Sagini alisema kuwa mwaka huu imekuwa ni tofauti na miaka mingine kutokana na kuwa taasisi nyingi zimejipanga kuonyesha uwezo wa hali ya juu kwa kwa wananchi wa mkoa huo.
 
“Mwaka huu kumekuwa na fursa vyingi ambazo miaka yote miwili iliyoita haikuwai kujtokeza kwani elimu imekuwa nyingi hivyo naamini wananchi wa Simiyu watanufaika sana na kile kilichopo kwenye maonyesho hayo”Alisema Sagini.
Mmoja wa wauzaji wa Dagaa wasio na michanga akimuelezea Sagini jinsi ya kuanika dagaa hao pasipo kuwa na michanga.(SHUSHU JOEL)
Aliongeza  Taasisi mbalimbali zikiwemo za serikali na zile za watu binafsi zimejitokeza kwa wingi kuonyesha kile walichonacho kwa wananchi wa Simiyu.
 
Kwa upande wake Bi,Bertha Nyambuko mara baada ya kutembelewa kwenye banda alisema kuwa mwaka huu kuna mabadiliko makubwa ikilinganishwa na kipindi cha nyuma kwani suala la maonyesha lilikuwa geni kwa wananchi wa maeneo hayo kwani inaonekana walizoea magulio lakini kipindi wakazi wengi wanajitokeza kwenye maonyesho na wengi wananunua na kuulizia vitu.
Sagini akiangalia viatu kutoka kwa mjasiliamali na mtengenezaji wa viatu(SHUSHU JOEL)
Aliongeza kuwa viongozi wa mkoa huu nao wamekuwa wabunifu siku hadi siku hivyo ni lazima tu watu wajae.
 
Naye Dotto Luhende ambaye ni Afisa Masoko wa Taifa Gesi alisema kuwa kipindi hiki kimekuwa na manufaa makubwa kutokana na kuwa wananchi wemekuwa na mwamko mkubwa wa kujua thamani ya maonyesho haya.
Mh sagini akipata maelezo ya jinsi ya kufukuza ndege kwa njia ya kisasa kutoka kwa wataalamu wa kutengeneza vifaa hivyo toka chuo kikuu cha Dar es Salaam(NA SHUSHU JOEL)
Aidha Luhende aliongeza kuwa kama inawezekana maonyesho hayo yakaendelea mkoa huu ni vyema zaidi kuliko kila baada ya miaka3 yanahama kwani hapa kwenye viwanja hivi kuna uwekezaji mkubwa umefanyika hivyo serikali ilione ili.
 
MWISHO

Post a Comment

0 Comments