MASWA YAWA KIVUTIO NANE NANE KWA KILIMO NA UFUGAJI.

Na Shushu Joel,Simiyu.

HALMASHAURI ya wilaya ya maswa ya Mkoani Simiyu imezidi kujizolea umaarufu kwenye sherehe za maonyesho ya nane nane yanayoendelea mkoani humo kwa kwa ufugaji wa samaki,Ng’ombe na kilimo cha Pamba.

Baadhi ya wananchi kutoka sehemu mbalimbali wakiangalia ufugaji wa samaki wa kisasa kwenye maonyesho ya nane nane mkoani Simiyu(NA SHUSHU JOEL)
Umaarufu huo unatokana na kumiminika kwa wakazi wengi kutoka sehemu mbalimbali kuingia kwenye banda hilo ili kujionea jinsi wilaya hiyo inavyofanya na kufanikiwa katika sekta hizo.


Akizungumza na baadhi ya wakazi waliojitokeza kujionea ufugaji wa samaki Afisa Uvuvi Salum Mazige alisema kuwa samaki ni moja ya utajiri mkubwa ambao unaweza ukabadilisha maisha ya mtu kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine  kwa haraka sana

Afisa Uvuvi wa wilaya ya Maswa Salum Mazige akitoa elimu kwa wananchi waliojitokeza kwenye maonyesho ya Nane Nane mkoani Simiyu(NA SHUSHU JOEL)
Hivyo mtaalamu huyo wa uvuvi kutoka wilaya ya Maswa amewataka watanzania kuendelea kuja maswa hata mara baada ya nane nane kumalizika ili kuja kujifunza namna ya ufugaji bora wa samaki.

Aliongeza kuwa ufugaji wa samaki kwa kipindi hiki unaumuhimu sana kutokana na kuwa samaki wana nyama nyeupe ambayo imekuwa ikisisitizwa na wataalamu wa afya kuwa ndiyo nyama ambayo haisababishi magonjwa kama zilivyo nyama yingine.

Moja ya Ng'ombe wanaopatikana katika wilaya ya Maswa na wameletwa Nane Nane ili wananchi waweze kujionea wenyewe(SHUSHU JOEL)
Aidha alisema kuwa amekuwa akifarijika sana tangu kuanza kwa maonyesho haya kwani wananchi wengi wamekuwa wakipita pita kwenye banda hilo ili kujifunza namna ya ufugaji wa samaki.


Kwa upande wake Afisa mifugo wa wilaya hiyo Saba Kashilimu alisema kuwa Halmashauri ya wilaya ya Maswa imekuwa mstali wa mbele kwenye kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa ufugaji wa mifugo wa kisasa kwa lengo la kuondokana na umasikini.

Afisa Uvuvi akitoa elimu kwa wananchi

Alisema ilikuwa ni chnagamoto kubwa sana kwa wilaya yetu kuweza kuwaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kufuga ng’ombe wa kisasa na hasa chotala ambao ndio wenye faida kubwa ikiwemo za mazingira lakini kwa sasa elimu imekuwa na tija kubwa kwa wananchi wengi wa maswa kuelewa thamani ya kuwa na mifugo hao.

“Ng’ombe chotala wanafaida nyingi ikiwemo kutokupatwa na magonjwa ya milipuko hivyo tumekuwa tukiwashauri wananchi kutumia mifugo hiyo kwa makusudi ya kujikwamua kwenye umasikini”Alisema Kashilimu.


Aidha Kashilimu aliongeza kuwa maonyesho ya nane nane yamekuwa yakiwafungua macho wananchi hivyo kama inawezekana tunaiomba serikali iongeze muda wa maonyesho hayo kutokana na kuwa elimu kubwa imewafikia wananchi wa Simiyu kwa ujumla wake

Afisa kilimo wa wilaya ya Maswa akionyesha moja ya mazo yenye tija katika wilaya ya Maswa ambalo ni zao la Pamba.
Naye Peter Emanuel mkazi wa ukerewe ambaye ametembelea maonyesho hayo alisema kuwa amekuwa akiifuatilia wilaya ya Maswa kwenye vyombo vya habari hivyo fursa hii ya nane nane imemfanya kufika ili kujionea yale aliyokuwa akiyaona ni kweli Maswa ni wilaya inayohitaji pongezi kwani inafanya vizuri sana kwenye ufugaji na kilimo.

Alisema kuwa elimu aliyoipata kwenye banda la maswa atahakikisha inafika ukerewe ili nako waweze kujifunza na kutekeleza lile aliloliona huko.

MWISHO

 

Post a Comment

0 Comments