Na Shushu Joel,Bagamoyo
KAMPUNI ya simu za mkononi ya Airtel nchini imezindua huduma za mfumo wa mawasiliano kwa kutumia 4G kwenye mji wa kitalii wa Bagamoyo Mkoani Pwani kwa kusudi la kuboresha huduma za upatikanaji wa mawasiliano ya urahisi kati ya Data na mawasiliano ya kawaida.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bagamoyo Bi, Fatuma Latu akikata utepe wa uzinduzi wa huduma ya 4G(NA SHUSHU JOEL) |
“Kwetu sisi Wana Bagamoyo kuzinduliwa kwa huduma hii ni mafanikio makubwa hivyo wananchi niwaombe tuiunge mkono kampuni hii ya Airtel kutokana na kuwa imekuwa ni msaada mkubwa kwa jamii ya Bagamoyo”Alisema Mkurugenzi Latu.
Duka la kutoa huduma za 4G lililozinduliwa wilayani Bagamoyo(NA SHUSHU JOEL) |
Kwa upande wake Meneja Biashara wa Airtel kanda ya Pwani,Brighton Majwala alisema kuwa ni vyema wananchi wa wilaya ya Bagamoyo wakachangamkia fursa hii iliyojitokeza kwao ya uwekezaji wa masafa ya huduma za 4G. kwani bora na zenye spidi ya pekee.
Mkurugenzi wa halmashauri ya Bagamoyo akiteta jambo na baadhi ya viongozi wa AIRTEL mara baada zoezi la ukataji utepe. |
Naye Juma Haji ni mmoja wa wateja
waliojitokeza kwenye uzinduzi huo ameipongeza kampuni ya Airtel kwa kutambua
thamani ya wananchi wa Bagamoyo kwa kuwapelekea huduma iliyokuwa wakiisubili
kwa muda mrefu.
Pia amewataka wananchi kuchangamkia
fursa hizo kwani kwa hali hii mtandao wa Airtel utakuwa kwa kwanza kwa kasi kwenye
mawasiliano na Data.
MWISHO
0717913670
0 Comments