ASASI YA THE ASMA MWINYI FOUNDATION YASHUSHA NEEMA KWA WANAFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUMU.

Na Shushu Joel,Dar

ASASI isiyo ya kiserikali ya The Asma Mwinyi Foundation imetoa misaada kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum katika shule ya msingi ya Uhuru mchanganyiko iliyoko Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuwasaidia wanafunzi hao kuweza kuendelea na masomo yao kwa vitendo kama ilivyo kawaida yao.

Mkurugenzi wa Asasi ya The Asma Mwinyi Foundation kulia akikabidhi kifaa cha kuandikia wanafunzi wenye ulemavu wa macho(NA SHUSHU JOEL)

Akizungumza wakati wa zoezi la kukabidhi vifaa hivyo Mkurugenzi wa Asasi hiyo Bi,Asma Mwinyi alisema kuwa Asasi hiyo imekuwa ikipambana na utatuzi wa changamoto mbalimbali katika mashule ya wanafunzi wenye mahitaji maalum ili waweze kupata mahitaji yao kama wanavyopata wengine katika uendelezaji wa elimu hapa nchini.


“Asasi yetu imejikita Zaidi kwenye kutoa misaada ya aina mbalimbali ikiwemo vifaa kama tulivyokabidhi leo kwa wanafunzi wa shule ya msingi uhuru ili kuwaondolea wanafunzi hao changamoto hizo”Alisema Mkurugenzi huyo wa Asasi hiyo.

Baadhi ya wanafunzi wakiteta jambo na Mkurugenzi wa The Asma Mwinyi Foundation mara baada ya kukabidhi vifaa maalum vya kusomea na kuandikia kwa walemavu wa macho

Aidha aliongeza kuwa changamoto ni nyingi na zote zinahitaji kutatuliwa ili wanafunzi hao nao waweze kujisikia wanatendewa haki kama wengine  lakini kupitia  kwa Asasi yetu imefanikiwa kutoa vifaa vinavyotumika kuandikia maneno ya Nukta Nundu kwa wanafunzi ambao ni walemavu wa macho waliopo katika shule hiyo.


Mbali na kutoa misaada hiyo Mkurugenzi huyo wa The Asma Mwinyi Foundation amewataka wananchi walio na uwezo kuendelea kujitolea kwa wahitaji ili kuwapunguzia mahitaji yanayowakabili ili kuisaidia serikali.


Kwa upande wake msimamizi wa wanafunzi wenye ulemavu katika shule hiyo Bw, Ahmed Abdallah ameipongeza Asasi hiyo kwa jinsi ambavyo imekuwa msaada mkubwa kwa shule hiyo kwani imekuwa ikijitolea mara kwa mara kwenye shule yetu.

Mkurugenzi wa Asasi ya The Asma Mwinyi Foundation akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko ambao ni walevu wa viungo mbalimbali.(Picha na Shushu Joel)

Aliongeza kuwa shule yetu ilikuwa na changamoto za vifaa vya wanafunzi kuandikia yaani Nukta Nundu lakini kupitia Asasi ya The Asma Mwinyi Foundation tumepokea vifaa 30 hivyo msaada huu ni mkubwa sana kwa shule yetu.


Naye mmoja wa wanafunzi wa shule hiyo Alphonce Wilbert ameishukuru Asasi hiyo kwa misaada hiyo ya vifaa vya kuandikia kwani walikuwa na changamoto kubwa lakini Asasi ya The Asma Mwinyi Foundation imekuwa msaada mkubwa kwetu kwani mahitaji yalikuwa ni makubwa kwetu.

MWISHO

Post a Comment

0 Comments