Na Shushu Joel

JUMUIYA ya Umoja wa Wanawake (UWT) Mkoa wa Pwani wamefurahishwa na utendaji kazi uliotukuka wa Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo  Bi Farida Mgomi.

Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Pwani Farida Mgomi  akiongoza wajumbe na  wanachana wa chama cha mapinduzi  kuchimba msingi wa shule ya Sekondari katika wilaya ya Mkuranga(NA SHUSHU JOEL)

Wakizungumza kwa wakati tofauti tofauti baadhi ya wanawake Mkoa huo walima kuwa tangu kuchaguliwa kuwa mwenyekiti Mgomi amekuwa msaada mkubwa na kimbilio la wanawake katika jumuiya hiyo.

Mwajuma Ally ni mkazi wa Kisemvule mara baada ya kuhojiwa na Mwandishi wa HABARI MPYA BLOG alisema kuwa awali jumuiya hii ilionekana kama vile imekufa katika mkoa wetu lakini tangu kuongoza  kwa Farida Mgomi kumekuwa na mabadiliko makubwa katika Nyanja za kimaendeleo ndani nan je ya jumuiya hiyo


Aliongeza kuwa Mwenyekiti amekuwa msaada mkubwa katika jamii na hasa katika mahusiano ya jumuiya na wananchi mbalimbali yamekuwa yakizidi kuimalika siku hadi siku.


“Nakumbuka kipindi cha kampeni cha chama chetu kilipokuwa kikisaka dola Mgomi akulala kwa kuhakikisha waliokuwa wagombea wa chama chetu wanashida na hili lilifanikiwa kwa asilimia mia”Alisema


Kwa upande wake Habibu Khaji amesifu utendaji wa Mwenyekiti huo kwani amekuwa akijitolea ku;liko wenyeviti wote ambao wamefanya kazi ya nafasi hiyo kwenye Mkoa wa Pwani.

Hivyo amemtaka Mgomi kuendelea kufanya kazi za jumuiya kwa kuwatetea wanyonge  ambao ndio wenye jumuiya yao.

Farida Mgomi Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Pwani akipiga chepe kutoa mchanga kwa ajili ya ujenzi wa moja ya shule za Sekondari katika kata ya vikindu wilaya ya Mkuranga(NA SHUSHU JOEL)

Akizungumza kwa njia ya simu Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo (UWT) Farida Mgomi alisema kuwa watu ndio wanaoona juhudi zake za utendaji wa kazi hivyo wanahaki ya kusema kwa kile wanachofanyiwa na viongozi wao.


“Jumuiya imekuwa ikifanya kazi mbalimbali za kijamii nah ii ni kutokana na kutokukaa ofisini na sasa tunawafuata wanyonge walipo tupo”Alisema Mgomi.

MWISHO

Post a Comment

0 Comments