Na Shushu
Joel,Kibaha Vijijini
MBUNGE wa Kibaha Vijijini Michael Mwakamo amefanikiwa kukamilisha ahadi yake ya kuwatengenezea vitambulisho vya matibabu wazee katika jimbo hilo ili kuondokana na changamoto iliyokuwa ikiwakabili awali.
Mbunge wa jimbo la kibaha vijijini Mhe:Michael Mwakamo akimkabidhi kitambulisho mmoja wa wazee kwa ajili ya matibabu.
Akizungumza wakati wa
utoaji wa vitambulisho hivyo Mwakamo amewataka wazee kuhakikisha wanavitumia
vitambulisho hivyo kama ilivyokusudiwani kwani dhamira yake ni kuwaondolea
wazee hao kupanga panga foleni pindi wanapokwenda kupatiwa matibabu.
“Sitaki kuona mzee yeyote Yule ndani ya jimbo hili kuona anateseka na matibabu ndio maana nimeamua kutoa pesa yangu ili kufanikisha zoezi la nyie kupatiwa huduma bure”Alisema Mwakamo
Baadhi ya wazee wakimsikiliza mbunge wakati akihutubia kabla ya kuwakabiidhi vitambulisho vya matibabu bure.
Aidha aliongeza kuwa
endapo ikitokea mzee anapatiwa manyanyaso ya aina yeyote ile katika shughuli za
huduma za basi mtu huyo anayefanya hivyo hatakuwa hajielewi maana naye ni mzee
mtarajiwa.
“Leo tumewakabidhi vitambulisho vya matibabu wazee 209 wa kata ya Ruvu tu ingawa bado wataalamu wanaendelea na utengeneaji wa kata nyingine lengo lengu ni kuwakabidhi wazee wote wa jimbo waoatao 500 hivyo huu ni mwanzo tu nitaendelea kila kata mara tu idadi ya kata Fulani inapokamilika”Alisema Mwakamo.
Naye mmoja wa wanufaika wa
vitambulisho hivyo Ndugu Adam Panjinga amempongeza mh Mbunge kwa msaada mkubwa
alioutoa kwa wazee wa jimbo hilo ambao walipata shida juu ya kupata huduma za
Afya.
Aidha aliongeza kuwa jambo
hilo la kupata huduma za matibabu kwa kutumia vitambulisho vya uzee.
“Jambo hilo utolewa na
serikali lakini kwa jimbo letu mbunge wetu ameamua kujitolea ili wazee wake
tuweze kuondokana na changamoto ya matibabu kwenye sehemu za utoaji wa huduma
za Afya”Alisema.
Naye Mganga mkuu wa
mlandizi Dr Ibrahim Isack ametumia muda huo kuwataka waganga wafawidhi kwenye
vituo vyote ndani ya wilaya hiyo kuhakikisha wanawapatia kipaumbele wazee wote
wanaofika kwenye vituo vya Afya kwa ajili ya matibabu.
MWISHO
0 Comments