RC KUNENGE WAANDISHI WATETA MAZITO

Na Shushu Joel,Kibaha

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali walio katika mkoa huo wamekutana ofisini kwa mkuu huyo wa mkoa kwa lengo la kutengeneza mikakati ya kufanya kazi za kuhakikisha mkoa huo unatangazika kutokana na upekee wa vitu vilivyo ndani ya mkoa wa Pwani.

Mkuu wa Pwani Abubakar Kunenge akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari(NA SHUSHU JOEL)

Akizungumza na wana hbari hao Kunenge alisema lkuwa Mkoa wetu umebalikiwa kuwa na kila kitu ambacho mikoa mingine na hata nchi jirani hawana hivyo niwaombeni wana habari kutumia taaluma yenu kuhakikisha mna wahabarisha wananchi ili waweze kujua kile kilichopo ndani ya mkoa wao.

“Niwashukuru kwa kuitikia wito huu kwani ni ngumu kuwapata waandishi wote na hii ni kutokana na wingi wa kazi zenu lakini mmeitikia wito kweli naamini mmenipa heshima kubwa sana mkuu wenu wa mkoa name sitowaangusha katika shughuli zenu za kila siku”Alisema Mkuu wa Mkoa Kunenge.

Aidha aliongeza kuwa mkoa wa Pwani una kila sababu ya kuwa namba moja kitaifa kutokana na uwepo wa kila kitu katika Nyanja karibia zote.

Kwa upande wake  Mohamed Nandonde mwandishi wa habari wa EATV amempongeza mkuu huyo wa Mkoa kwa kutambua thamani ya waandishi na hata kuamua kufanya kikao kwa ajili ya kujadili jinsi gani mkoa wa Pwani utakavyotangazwa na wana habari hao kupitia vyombo vyao vya habari.

Aidha aliongeza kuwa ni kweli mkoa wa Pwani una kila sababu ya kuwa kinara katika kila Nyanja kutokana na jinsi mkoa huo ulivyo jipambanua kwani viwanda ni vingi,mazao meni mengi na kila kitu kipo kwenye mkoa huu wa Pwani.

Naye Monica Samba ni mwandishi wa habari wa star Tv alisema kuwa ni vyema sasa kila mwandishi akajipambanua na kutumia fursa iliyotolewa na mkuu huyo wa mkoa kwa waandishi wote wa mkoa wa Pwani.

MWISHO

 

Post a Comment

0 Comments