SONGE AWATAKA WANAFUNZI KUSOMA MASOMO YA SAYANSI.

Na Shushu Joel,Busega.

MBUNGE wa Jimbo la Busega Mkoani Simiyu Mhe:Simon Songe amewataka wanafunzi kuchangamkia nafasi ya  kusoma masomo ya sayansi kwa kusudi la kuja kulitumikia taifa letu kwa weredi wa hali ya juu.

Mbunge wa Jimbo la Busega Mh: Simon Songe akizungumza na waWanafunzi wa kidato cha sita katika shule ya sekondari Mkula(NA SHUSHU JOEL)

Sayansi ni masomo mepesi sana kuliko masomo mengine na hasa somo la Hesabu pia ni masomo yenye kuhitajika sana kutokana na uchache wa watu waliosoma masomo hayo katika taifa letu na hasa kwenye kipindi chenu,hivyo niwaombeni kila mmoja wenu kuchangamkia fursa ya kusoma masomo ya sayansi


Aliongeza kuwa serikali ya Rais wetu mpendwa Samia Suluhu Hassani imejikita kwenye kujenga maabara za aina tatu kwa kila shule ambazo ni biologia,kemia na physicia kwa kusudi la kuwawezesha wanafunzi kutokupata changamoto ya aina yeyote ile pindi mnapojifunza masomo hayo kwa  vitendo.

“Someni masomo ya sayansi kwani yana uharaka wa upatikanaji wa ajira hivyo hii ni fursa kwenu wanafunzi wa Busega”Alisema Mhe: Songe

Aidha Songe amewataka wanafunzi wote wa jimbo hilo kuhakikisha wanaongeza bidii katika kujisomea kwani elimu ni mtaji wa elimu na elimu nzuri inaanzia hapa mlipo sasa.

“Shule yetu ya mkula imekuwa miongoni mwa shule kumi bora zilizofanya vizuri kwa wanafunzi wa kidato cha sita hivyo na nyie mpambane muwazidi watangulizi wenu kwani sie wazazi wenu furaha yetu ni kuona nyie mkifanya vizuri kwenye masomo yenu”Alisema Songe.

Kwa upande wake Mwajuma Ally ambaye ni mwanafunzi wa kitado cha sita amemwakikishia mbunge kuwa wao wamejipanga kufanya vizuri zaidi ya watangulizi wao.

Pia wamempongeza mbunge kwa juhudi zake za kuhakikisha shule hiyo ya Mkula inakuwa na michepuo yote yaani sayansi na hati.

Baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari Mkula wakimsikiliza Mbunge wa jimbo la Busega Simon Songe (NA SHUSHU jOEL)

Naye Ngwashi Ibrahimu ni miongoni mwa wanafunzi wa kidato cha tano waliochaguliwa mwaka huu alisema kuwa Mhe: Songe ni mbunge wa pekee kwani ametufariji sana wanafunzi na kututia moyo kwa ajili ya kusomo kwa bidii ili baadae kuja kulisaidia taifa letu.

Aidha aliongeza kuwa uwepo wa maabara kutafungua fursa kwa wanafunzi wote yaani wale wa kidato cha kwanza mpaka cha nne kuweza kujifunza kwa vitendo na hata baadae wale wa kidato cha tano na sita wakianza kusomo masomo hayo katika shule yetu kutakuwa na wasomo wa pekee katika shule ya Mkula sekondari.

MWISHO

Post a Comment

0 Comments