WLC YAJA NA MIKAKATI KABAMBE YA USAFIRISHAJI MIZIGO KIPINDI CHA UVIKO 19

 Katika kukabiliana na wimbi la tatu la Uviko 19  kampuni ya usafirishaji wa mizigo  ya   World Logistics company (WLC, )imezindua huduma ya kusafirisha mizigo ili kumfikia mteja kwa urahisi  ijulikanayo Cargo Pickup Delivery Service.

Mkuu wa kitengo Cha masoko bi Agnes wa kwanza kushoto akizungumza na waandishi wa habari

Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es salaam Mkuu wa kitengo cha Masoko wa kampuni hiyo Agnes Daniel alisema kuwa huduma hiyo inatarajia kumuhakikishia Muagizaji na Mpokeaji kuepuka usumbufu na gharama za usafiri na zinginezo.

"Huduma  hii itamsaidia anayeagiza mizigo kuepuka usumbufu nakuepuka gharama zinginezo  nakubaki Salama dhidi ya  ugonjwa wa Uviko 19,. Alisema Agnes Daniel.

Agnes alisema kuwa  kupitia teknojia Muagizaji ataweza kufuatilia mzigo wake katika hatua zote za usafirishaji za mizigo kuanzia siku yakwanzaalipoagiza Mzigo na kupokeamzigo huo kwa kutumia nyenzo ya  Google Excle.

Aliongeza kuwa tofauti ya nyinginezo za usafiri shaji kampuni hiyo imejikita kufanya shughuli zake kupitia teknolojia hiyo.

MWISHO

Post a Comment

0 Comments