“WATANZANIA MACHO YOTE PWANI KUMALIZA KATIKA KATIKA YA UMEME” RC KUNENGE

Na Shushu Joel,Pwani

KUTOKANA na changamoto inayoendelea kutokea nchini kwa baadhi ya sehemu kukosa huduma muhimu ya nishati ya umeme na kupelekea kupungua kwa ufanisi wa baadhi za kazi kwa wananchi mbalimbali ambao wamekuwa wakifanya shughuli zao kwa uhitaji wa umeme.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akiteta jambo na Mbunge wa jimbo la Chalinze mara baada ya kutembea mradi wa ujenzi wa mradi wa Umeme wa Mwalimu Nyerere(NA SHUSHU JOEL)

Aidha Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amewataka wananchi wa Mkoa huo na Watanzania kwa ujumla kuendela kuwa na subra kwani serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imejipanga kikwelikweli kwa kusudi la kuhakikisha Tanzania inakuwa nchi ya pekee Afrika Mashariki kwa uhakika wa upatikanaji wa uhakika wa Umeme.

“Mpaka sasa mradi huo wa mwalimu Nyerere unaendelea vizuri katika ujenzi na muda si mwingi watanzania wataanza kunufaika na mradi huo mkubwa ambao unajengwa kwa fedha za ndani, hii ni hatua kubwa sana kwa Taifa letu kwa kutumia pesa za ndani kutekeleza miradi mikubwa ambayo ni faida kubwa kwa watanzania”Alisema Kunenge

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa wa Pwani alisema kuwa kuwepo kwa mradi huo katika Mkoa wa Pwani umefungua fursa nyingi kwa vijana na wananchi kwa ujumla kwani wananchi wameweza kunufaika kwa kupata ajira katika nafasi mbalimbali kwenye mradi huo uligharimu kiasi kikubwa cha fedha.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa aliongeza kuwa mara baada ya kukamilika kwa mradi huo utaenda kumaliza kabiza changamoto ya katika katika ya umeme pia Taifa litaingiza fedha nyingi za kigeni kutokana na uzalisha wa umeme huo kuwa mkubwa kuliko uhitaji wetu.

Kwa upande wake mmoja wa wananchi ambaye ni mkazi wa Mkoa wa Morogoro Juma Mahina alisema kuwa pindi mradi huo utakapo kamilika utasaidia Taifa letu kwa asilimia mia.

Aliongeza kuwa mradi wa Mwalimu Nyerere ukikamilika utaenda kujenga ajira nyingi kwa watanzania kwani umeme ni mtaji mkubwa na huu ni umeme wa uhakikia hivyo wananchi wanaenda kuwa wenye kipato cha kuridhisha mara baada ya kuanza kutumika kwa mradi huo.

Aidha Mahina aliongeza kuwa ni vyema serikali ikawekeza nguvu nyingi za usimamizi ili mradi huo ukamilika kwa muda ili kuokoa katika katika ya umeme ambao umekuwa ukijitokeza kwa sababu mbalimbali.

Naye Mariamu Ally mkazi wa Simiyu mara baada ya kuzungumza na Mwandishi wa Habari wa HABARI MPYA BLOG alisema kuwa wao wanausubili mradi huo kwa hamu kwani ni mkombozi wetu.

Aidha aliongeza kuwa pongezi ziende kwa serikali ya Mkoa wa Pwani chini ya Abubakar Kunenge ambaye amekuwa mstali wa mbele kama Mkoa kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa haraka ili kusaidia Taifa kwenye Nyanja ya Nishati.

“Awamu ya sita ni serikali sikivu na yenye uchu ya kuona wananchi wake wanapata miradi mikubwa kwa fedha za ndani hivyo Rais Samia Suluhu HJassani ni jembe letu tunalolitegemea kutuvusha hapa tulipo “

MWISHO

 

 

 

 

 

Post a Comment

0 Comments