“UONGOZI NI KUACHA ALAMA”MWENYEKITI WA WAZAZI PWANI

Na Shushu Joel, Kibaha

MWENYEKITI wa jumuiya ya wazazi Mkoa wa Pwani Jackson Kituka amewakumbusha viongozi wa jumuiya hiyo katika wilaya ya Kibaha  kuhakikisha wanaacha alama katika nyadhifa zao za uongozi kwa wananchi wanaowaongoza.

Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi Mkoa wa Pwani Jackson Kituka akiteta jambo na mmoja wa viongozi wa jumuiya hiyo wilaya ya Kibaha mara baada ya kikao maalum(NA SHUSHU JOEL)

Hayo ameyasema alipokuwa akizungumza na viongozi wa jumuiya hiyo katika wilaya ya Kibaha ambapo amewasisitiza kuwa kiongozi bora ni Yule anayesimamia miongozo kwa ajili ya kuisaidia jamii anayoiongoza

“Wengi tumekuwa na mawazo tofauti juu ya uongozi hivyo nawaombeni viongozi wezangu tuweze kujitolea kwa dhati kwa wananchi wetu ili kuweza kuweka alama kwa wananchi wetu”Alisema Kituka

Aidha Mwenyekiti huyo aliwakumbusha viongozi wa jumuiya hiyo kuwa wazazi ndio nguzo kubwa katika jumuiya zote za chama cha mapinduzi hivyo ni lazima kila kiongozi kuonyesha ukomavu wake ili jumuiya zingine ziweze kujifunza kupitia wazazi.

“Rais wetu amekuwa akitenda mambo mengi mema kwa jamii na hasa yale ya kimaendeleo kwa watanzania hivyo ni muhimu sie kama wazazi kuhakikisha tunakuwa mstali wa mbele kwenye kubeba yale yote yanayofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan”Alisema Mwenyekiti huyo wa jumuiya ya wazazi Mkoa wa Pwani.

Aidha aliongeza kuwa matamanio yangu ni kuona kila kiongozi wa jumuiya ya wazazi kuanzia ngazi ya shina mpaka kata anakuwa kiongozi wa kuigwa kwa kuweka alama za uongozi kwa jamii.

Mwajuma Mohamed amempongeza Mwenyekiti huyo kwa juhudi zake anazozifanya kwa wana chama kwa kusudi la kuwaweka pamoja na kuwakumbusha wajibu wao kila mmoja wetu.

Aliongeza kuwa kiongozi unapoweka alama ya uongozi unakuwa ni mfano mkubwa kwa jamii hivyo maneno ya Mwenyekiti ni ya kuigwa kwa viongozi wote.

MWISHO

Post a Comment

0 Comments