RC KUNENGE ATOA AGIZO KWA WAVUNAJI MISITU HOLELA.

Na Shushu Joel,Pwani

 

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amepiga marufuku uvamizi na  uvunaji holela wa miti  kwenye maeneo ya vijiji,vyanzo vya maji na misitu ya hifadhi kwani kuna watu wamevamia kwenye hifadhi na kufanya uharibifu mkubwa kwenye misitu kitu ambacho kinapelekea kutishia uendelevu wa hifadhi ya mazingira na vyanzo vya maji.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akisisitiza jambo(NA SHUSHU JOEL)

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Kunenge alisema kuwa tabia hizo za ukataji wa miti ovyo kumepelekea kuwepo kwa changamoto nyingi za kitabia ya nchi hivyo niwatake wale wote wanaojishughulisha na kazi hizo kuacha mara moja.

 

“Sheria ya misitu Na 14 sura ya 323 iliyorejeshwa mwaka 2022,taratibu na kanuni za misitu za mwaka 2004 tangazo la serikali (GN) Na 417 la mwaka 2019, Na 59 la mwaka 2022 na mwongozo wa uvunaji endelevu na biashara ya mazao ya misitu wa mwaka 2017 vinaelekeza uvunaji wa mazao ya misitu” Alisema Mkuu wa Mkoa.

Aidha alisema kuwa ni vyema sasa wale wote wanaoendeleza uvunaji holela katika maeneo ya misitu katika Mkoa wa Pwani wahakikishe wanaacha mara moja tabia hiyo kwa kusudi la kulinda misitu.

Mbali na agizo hilo Mkuu wa Mkoa huyo amewataka waandishi wa habari wa Mkoa huo kuhakikisha wanatumia kalamu zao kufikisha ujumbe kwa jamii ambazo zimekuwa na tabia ya kuvamia misitu holela.

MWISHO

 

Post a Comment

0 Comments