WAANDISHI WA HABARI PWANI WAPIGWA MSASA JUU YA COVID 19.

Na Shushu Joel,Pwani.

WAANDISHI wa habari Mkoa wa Pwani wamepewa elimu juu ya umuhimu wa kuelimisha jamii  jinsi ya kujikinga na maambukiza ya  ugonjwa wa COVID 19

Waandishi wa habari wa Mkoa wa Pwani wakijengewa uwezo juu ya masuala ya kuandika hbari za COVID 19 na aliyesimama ni Mganga Mkuu wa Mkoa huo Dr. Gunini Kamba(SHUSHU JOEL)


Akitoa elimu hiyo kwa waandishi wa habari wa Mkoa huo Dr, Caroline Akim kutokea WHO  alisema kuwa waandishi ni jeshi kubwa lenye uwezo wa kufikisha taarifa za haraka kwa umma hivyo ni jambo la muhimu sana kuwaelimisha waandishi kwa kusudi la kuisaidia jamii.

Aidha aliongeza kuwa ugonjwa huu umekuwa na changamoto kubwa kwa jamii lakini kutokana na juhudi mbali mbali ambazo zimekuwa zikichukuliwa na serikali mapambano yamekuwa ni makubwa ili kuwasaidia wananchi wa Taifa husika.

 “Ugunduzi wa chanjo umekuwa ni msaada mkubwa kwa watu ndio maana hata miaka ya nyuma palipogundulika chanjo ilifanikiwa kuzuia chanjo kwa watoto na ndio maana hata ujio wa chanjo ya COVID 19 imeleta matokea chanya  kwa  jamii  hivyo chanjo ni muhimu sana na  jamii husika  iendelee kupata chanjo ili kuondokana na magonjwa kama hayo” Alisema Dr Akim

Pia alisema kuwa chanjo zote zilizopo nchini ni salama na zina faida kubwa kwa wananchi hivyo zoezi hili la kupata chanjo liendelee ili kuepuka usumbufu pindi mtu anapoambukizwa ugonjwa huo.

Aliongeza kuwa lengo kubwa la kuanzishwa kwa chanjo hiyo ni kwa ajili ya kuwakinga wananchi dhidi ya ugonjwa huo wa Covid 19 hivyo kusudi ni kuhakikisha watanzania wote wanapata chanjo ili kuepukana na maambukizi ya ugonjwa huo.

“ Tuwaombe waandishi wa habari kuhakikisha wanatumia kalamu zao vyema kwa kusudi la kuisaidia jamii juu ya umuhimu wa upataji wa chanjo”Alisema Dr Akim


Aidha aliongeza kuwa mpaka sasa takwimu za ugonjwa wa COVID 19       zinaonyesha kuwa watanzania waliopata ugonjwa huo ni 38,205 na vifo mpaka sasa ni watu 845.


Kwa upande wake mmoja wa waandishi wa habariwalioshiriki katika semina hiyo  Gustaph Haule   ameipongeza WHO kwa kutambua umuhimu wa waandishi wa habari katika jukumu la kuielimisha jamii kupitia  vyombo mbali mbali vya habari.


 Aidha alisema kuwa waandishi wako tayari kuisaidia serikali katika suala zima la utoaji elimu kupitia taaluma zao.


Pia amewataka waandishi kuhakikisha wanayatumia mafunzo ya COVID 19 kama chachu ya usambazaji wa elimu kwa jamii ili waweze kupata chanjo na kujiongezea kinga katika miili yao.

MWISHO

 

 

Post a Comment

0 Comments