KIKWETE AWATAKA WANANCHI KUCHANGAMKIA HATI MILIKI.

Na Shushu Joel, Dar

Naibu Waziri wa Ardhi akisisitiza jambo mbele ya warasimishaji wa Ardhi

NAIBU Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Ridhiwani Kikwete amewakumbusha wananchi kuhakikisha wanachukua Hati miliki za maeneo yao ili ziweze kuwasaidia katika mambo mbalimbali ikiwemo hata kukopesheka kwa ajili ya kukuza biashara zao.


Rai hiyo ameitoa alipokuwa kwenye mkutano na makampuni yanayofanya kazi y urasimishaji katika Mkoa wa Dar es Salaam.


“Mwananchi unapokuwa na hatimiliki yako inakuwezesha kuwa na faida kubwa sana na eneo lako kutokana na kuwa na hati zako hivyo inakufanya kukopesheka kwenye taasisi mbalimbali za kifedha kitu ambacho kitapelekea kuinua uchumi wako” Alisema Kikwete.


Aidha kikao hicho kimeudhuliwa na kamishina msaidizi Mkoa wa Dar es Salaam Shukrani Kyando.

MWISHO

Post a Comment

0 Comments