NAIBU WAZIRI KHAMIS ATAKA WAFUGAJI WATUNZE VYANZO VYA MAJI

 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis

Hamza Khamis ametoa rai kwa wafugaji nchini kuzingatia hifadhi ya mazingira

kwa kutoharibu vyanzo vya maji.


Ametoa rai hiyo  wakati wakati wa Kongamano la Wadau

Sekta ya Mifugo lililofanyika jijini Dodoma na kufunguliwa na Waziri Mkuu Mhe.

Kassim Majaliwa.


Amesema kuwa kwa mujibu wa utafiti wa kimazingira, sehemu kubwa ya

uchafuzi wa mazingira inatokana na shughuli za kibinadamu zikiwemo kilimo

kisicho endelevu, ufugaji usio endelevu na uchimbaji wa madini usiofuata sheria

za mazingira.


Mhe.Khamis amesema pamoja na kuwa ufugaji ni sekta kubwa inayokuza

uchumi na kutangaza nchi yetu wafugaji wanao wajibu wa kuhakikisha

wanafuata sheria za mazingira.


“Niwaombe ndugu zangu wafugaji tuhakikishe hatuchungi wala hatunyweshi maji

mifugo yetu kwenye vyanzo vya maji kwani kwa kiufanya hivyo tutasababisha

uharibifu wa mazingira na kuua viumbe waishio humo,” aalisema.

Aidha, naibu waziri huyo amewasisitiza wafugaji na wananchi kwa ujumla

kupanda miti na kuitunza ili kusaidia kupambana na athari za mabadiliko ya

tabianchi yanayoikumba nchi yetu.


Amesema hali ni mbaya kwasababu maeneo mengi wananchi wamekata miti

ovyo hali inayosababisha ukosefu wa mvua na hivyo ukame kukithiri katika

maeneo mbalimbali ya nchi.


Naibu Waziri Khamis amesema kuwa mifugo inahama kutafuta malisho

kwasababu ukame unaosababishwa na ukosefu wa mvua uliochangiwa na

ukataji miti.


“Wakati tunapita na Kamati ya Mawaziri tumeona baadhi ya maeneo

yameakauka sana kwa sababu za kibinadamu zikiwemo kilimo, ufugaji au

uchomaji moto ovyo kwa ajili ya kuni na mkaa, niwashauri ndugu zangu pamoja

twendeni tukapande miti na kuishughulikia (kuitunza),” alisisitiza

Post a Comment

0 Comments