KATIBU UWT KIBAHA VIJIJINI AELEZA FAIDA ZA KUPANDA MITI.

 Na Shushu Joel, Kibaha 

Katibu wa UWT wilaya ya Kibaha Vijijini Nurath Mkandawile akipanda miti kuhamasisha wananchi kuendelea na zoezi hilo.(NA SHUSHU JOEL)

KATIBU wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT)  Wilaya ya kibaha vijijini Mkoani Pwani Bi Nurath Mkandawile ameikumbusha jamii kuendelea kupanda miti katika maeneo mbalimbali yanayowazunguka ili kuweza kuisaidia ardhi yetu iendelee kuwa na uoto wa baridi na wenye rutuba.


Rai hiyo ameitoa ofisini kwake  alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo vya habari mbalimbali. 


Mkandawile alisema kuwa kumekuwa na changamoto nyingi nchini kutokana na ukataji wa miti ovyo jambo ambalo limetusababishia kukosekana kwa uoto wa Asili pia ukosefu wa mvua ya kutosha kwa ajili ya kilimo.


Hivyo Katibu huyo wa UWT wilaya ya kibaha vijijini ameiomba jamii kupanda miti na kuitunza ili  iweze kuturudishia uoto wetu wa asili kama walivyokuwa wamefanya mababu zetu.


"Babu zetu waliitunza miti ndio maana walifanikiwa mambo yao kutokana na utunzaji wa mazingira ambao uliwapa neema kubwa ya uzalishaji wa mazao kutokana na kunyesha kwa mvua nyingi kutokana na uwepo wa miti"  Alisema Mkandawile 


Aidha alisema kuwa mbali na kupanda miti ni wajibu wetu kila mmoja wetu kuweza kuitunza miti hiyo kwa kusudi la kuleta tija kwa jamii zetu.


Naye Nikodemas Ally  amempongeza katibu hiyo kwa kutoa hamasa kwa jamii kuweza kupanda miti kwa kila mmoja ili kuweza kuondokana na joto lilipo sasa.


MWISHO

Post a Comment

0 Comments