MARIAM ULEGA ATOA SOMO KWA WANAWAKE

Na Shushu Joel,Mkuranga

MWENYEKITI wa Jukwaa  la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Mkoa wa Pwani Bi, Mariam Ulega amewakumbusha wanawake kuhakikisha wanaongeza juhudi za uwajibikaji ili waweze kujiongezea kipato ili waondokanae na umasikini.

Bi, Mriam Ulega ambaye ni Mwenyekiti wa jukwaa la wanawake Mkoa wa POwani (NA SHUSHU JOEL) 

Rai hiyio ameitoa alipokuwa Akizungumza na kundi la wanawake katika wilaya ya Mkuranga ambapo alisisitiza ili kuondokana na umasikini ni lazima Wanawake tuweze kujishughulisha na kazi mbalimbali ambazo zitatuongezea kipato chetu na si kile cha kutegemea kupewa.


“Wanawake ni jeshi kubwa hivyo inapotokea tunashikamana kwa pamoja ni lazima tuweze kufanya jambo kubwa na lenye manufaa makubwa kwetu wenyewe na jamii kwa ujumla” Alisema Mariam Ulega.


Aidha Mwenyekiti huyo amewakumbush Wanawake kuchangamkia mikopo inayotolewa na serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan iliyopo katika kila halmashuri hivyo mikopo hii itatusaidia kutuinua kuuchumi.


Aidha amewataka Wanawake kuendelea kuyasema yale yote mazuri yuanayofanywa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwenye Taifa hili.


Naye Khadija Juma amemsifu Mwenyekiti huyo kwa jinsi ambavyo amekuwa msaada mkubwa kwa Wanawake na jamii kwa ujumla.


MWISHO

Post a Comment

0 Comments