“RAIS DKT SAMIA MKOMBOZI WA WANAWAKE SEKTA YA MAJI” SUBIRA MGALU

Na Shushu Joel,Bagamoyo

MBUNGE wa viti maalum kutokea Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT)  Mkoa wa Pwani Subira Mgalu  amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuzidi kuendelea kutatua changamoto ambazo zilikuwa ni sugu kwa Wanawake hapa nchni,

MBUNGE wa viti maalum Mhe, Subira Mgalu akifurahi jambo na Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo mara baada ya uzinduzi wa mradi wa Maji ( NA SHUSHU JOEL)

Akizungumza katika uzinduzi wa mradi wa maji wa kata ya Fukayosi wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani Mgalu alisema kuwa Rais Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan amedhamilia kwa moyo wake wa dhati kuhakikisha wanawake wanaondokana na changamoto ya maji na badala yake wanajikita katika uzalishaji wa uchumi.

Aliongeza kuwa Wanawake wengi walikuwa ni wahanga wakubwa wa changamoto za ukosekanaji wa maji hivyo muda mwingi wamekuwa wakiutumia kutafuta maji na sio kutengeneza uchumi kitu hicho kimekuwa kikimuumiza kichwa sana Mhe. Rais ndio maana anazitatua kero hizo kila kukicha kwa kutoa fedha za miradi ya maji.

Mgalu alisema kuwa kukamilika kwa mradi wa maji katika kata ya Fukayosi unakwenda kuokoa uchumi wa wanawake wa Bagamoyo kwani wengi waliokuwa wakikesha kutafuta maji sasa wanakwenda kuzalisha uchumi wao kwani maji yako mlangoni na wanaanza kuchota bila wasiwasi.


“Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ni Mwanamke ndio maana amekuwa akipambana sana na chanagamoto hizo kutokana na kuwa hata yeye amezipitia hivyo anataka changamoto hizo ziishe kabisa na zibaki kuwa historia katika Taifa hili” Alisema Mgalu.

Aidha aliongeza kuwa mradi huu ni mkubwa hivyo ni jukumu letu wananchi kuulinda ili uweze kudumu kwa kipindi kirefu.

Naye Meneja wa Ruwasa Wilaya ya Bagamoyo James Kionaumela amesema kuwa mradi huo umegharimu kiasi cha shilingi Milioni mia tatu hamsini (350,344,596,00) zote zikiwa ni pesa ya serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Aliongeza kuwa Wanawake wanahaki ya kulinga sasa juu ya Rais huyu mwenye maono makubwa juu ya utekelezaji wa miradi ya maji kwani Rais ameamua kuwatua wanawake ndoo kichwani kwa dhati kabisa,

MWISHO

Post a Comment

0 Comments