Na Shushu Joel, Dar
MWENYEKITI wa Idara ya Wanawake na watoto kutokea shirikisho la vyama vya watu wenye ulemavu Tanzania ( Shivyawata) Bi, Nasirya Ally amempongeza Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake Mkoa wa Pwani Mariam Ulega kwa kukugwa na changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu na hata kuweza kuwawezesha kwa kuwasaidia mahitaji mbalimbali.

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake Mkoa wa Pwani Mariam Ulega Kulia akimkabidhi zawadi mwenyekiti wa Viziwi zawadi ( NA SHUSHU JOEL)
Akizunguimza
mara baada ya kukabidhiwa kwa zawadi za sale kwa wanawake ambao wanakwenda
kushiriki zoezi la sherehe za wanawake dunia Mwenyeki huyo wa Shivyawata
alisema kuwa Mariam Ulega amewafanya wajione wako juu kama ilivyo kwa wengine.
Aliongeza
kuwa tulikuwa na changamoto kubwa na ilipelekea kuonekana kuwa ni wanyonge
kutokana na ulemavu wetu lakini ujio na ugawaji wa zawadi hizi unakwenda
kufungua milango ya Mariam Ulega kwani amekuwa akijitoa sana kwa wahitaji wengi
hata sie kumpata ni Bahati lakini Mungu atamuongezea kwa pale alipotoa.
Aidha aliongeza kuwa kupitia Mariam Ulega tunawaomba watanzania wenzetu waweze kuiga mfano wa Mwanamke huyu ambaye kwetu ametuheshimisha sana wanawake viziwi.
Kwa upande
wake Mariam Ulega Mwenyekiti wa Jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi Mkoa wa
Pwani alisema kuwa kutoa ni moyo hivyo kila mtu mwenye nafasi namuomba aweze
kujitolea kwa wahitaji ili nao wajisikie kama tunavyojisikia sie.
Aidha
aliongeza kuwa unapowsaidia wahitaji wanajisikia vizuri sana hivyo tuendelee
kuwasaidia kwa mahitaji yao kwani hata sisi ni walemavu watarajiwa maana hakuna
mwenye kujua mipango ya Mungu wetu kuwa kesho utakuwa nani.
MWISHO

0 Comments