WAZAZI YAWAKUMBUKA WALEMAVU KWA KUWAPATIA WHEEL

Na Shushu Joel, Ilala.

MLEZI wa Jumuiya ya Wazazi Kata ya Ilala wilaya ya Ilala Mkoani Dar es Salaam Ndugu Imran Jaffer mewakabidhi baiskel za miguu mitatu walevu ili ziweze kuwasaidia katika shughuli zao za kila siku.



Akizungumza na HABARI MPYA MEDIA Imran alisema kuwa ameamua kujitolea na atazidi kuwa wananchi mahitaji maalum ili kuweza kuendani na serikali.


Alisema kuwa ni muhimu kujitoa kwa jamii na hasa kwa watu wenye uhitaji ili kuwawezesha nao kujiona wanapendwa na wana jamii wenzao.

Aidha Imran aliongeza kuwa ataendelea kujitoa kwa jamii ili aweze

kuwawezesha kupata mahitaji yao muhimu kutokana na kuwa yeye ni mtu wa jamii sana.



Kwa upande wake mmoja wa wapokeaji wa baiskel hizo za miguu mitatu ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema kuwa zawadi hizo zimekuja kwa muda sahihi kutokana na wengi wao kutokuwa na pesa za kununua baiskel hizo hivyo tutaendelea kumuombea dua Imran ili aweze kufanikiwa Zaidi ya hapo ili aweze kujitoa Zaidi

MWISHO

Post a Comment

0 Comments