Na Shushu Joel, Dar.
MJUMBE wa halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa kutokea wazazi ( MNEC) Hamoud Jumaa amewataka jumuiya ya Umoja wa Vijana wilaya ya Ilala Mkoa wa Dar es Salaam (UVCCM) kuendeleza jumuiya hiyo kwa misingi mikubwa iliyowekwa na viongozi waanzilishi wa jumuyiya hiyo.

MNEC Hamoud Jumaa akiveshwa skafu na vijana wa skauti wa Ilala mara baada ya kuwasili katika viwanja vya karinjee ( NA SHUSHU JOEL)
Rai hiyo
ameitoa nalipokuwa akizungumza na Vijana wa wilaya ya Ilala katika Mkutano wa
Baraza la umoja huo katika viwanja vya Karinjee ambapo amewakumbusha kuwa
Jumuiya hiyo iliundwa na CXCM kwa mahususi makubwa ili iweze kuwa msaada mkubwa
katika chama hicho.
Aliongeza
kuwa Jumuiya ya Vijana ni tanuru kubwa la kuoka viongozi kwa ajili ya kesho
ndani ya Chama Cha Mapinduzi na Serikali
kwa ujumla hivyo ni vyema kila mmoja wenu kuweza kutumia ujana wake vizuri ili
hapo baadae Taifa liweze kunufaika nanyi.
“Kumbukeni
na mimi nilikuwa kijana hapo zamani sasa hivi mie ni mzee sasa mnapaswa
kuendeleza maadili yaliyo mema kwa nchi yetu ili muwe walithi sahihi kama vile
mnavyoandaliwa na wazazi wenu” Alisema Hamoud Jumaa (MNEC)
Kwa upande
wake Albert Sweya ambaye ni mmoja wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya
ya Ilala amempongeza MNEC kwa ushauri wake kwa vijana ambao wengi wao
wameonekana kuwa na tamaa ya mafanikio ya haraka kitu ambacho kimekuwa
kikiwakwamisha wengi wao.
Aidha
amewataka vijana kutumia ushauri uliotolewa na kiongozi huyo ili kuweza
kulisaidia Taifa letu hapo kesho.
MWISHO
0 Comments