“ WANAFUNZI WATAKIWA KUFUNIKA VITABU VYAO” MWENYEKITI UWT ZAYNABU VULU.

Na Shushu Joel, Kibaha.

MWENYEKITI  wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa wa Pwani Bi, Zaynabu Vulu amewataka wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Wasichana ya Kibaha kutokufunua funua vitabu vyao kwa wanaume na badala yake wavifunike mpaka pale muda utakapofika.

Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Pwani Zaynabu Vulu akigawa taulo za kike kwa wanafunzi wa shule ya Wasichana Kibaha (NA SHUSHU JOEL)

Rai hiyo ameitoa alipokuwa akizungumza na wananfunzi wa shule hiyo ambapo amewasihi kutumia uanafuzi wai vizuri ili kutimiza ndoto zao ambazo kila mmoja amekuwa akijiwekea katika maisha yake.

Alisema kuwa ni vyema kila mwanafunzi kuweza kutambua thamani yake ya sasa na ndio maana hata Serikali ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan amekuwa akisisitiza juu ya Elimu kwa wasichana.

Aidha Mwenyekiti huyo amewagawia wanafunzi hao Taulo za kike kwa ajili ya kutunza mazingira ya usafi wa miili yao ili kuondoa changamoto wanazokutana nazo wakati wa hedhi.

Pia amewakumbusha Wananfunzi hao kutambua kile kilichowapeleka shuleni hapa kwani Taifa linawategemea ili baadae waje kuwa viongozi .


“ Niwakumbushe kutambua kuwa hata sisi tulikuwa wanafunzi kama mlivyo nyie leo hivyo ni vyema mkafunga vitabu vyenu ili baadae mje mchukue nafasi zetu hizi tulizonazo” Alisema Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Pwani Zaynabu Vulu.

Kwa upande wake mmoja wa wanafunzi wa shule hiyo Asha Juma ameupongeza uongozi wa UWT Mkoa wa Pwani kwa jinsi ambavyo umetoa elimu kwao kwa kuwakumbusha kutambua umuhimu wa kuzingatia elimu.


“ Tunawahakikishie kuwa hatutofunua vitabu vyetu na tutavitunza ili kutimiza malengo yetu ambayo yametuleta hapa shuleni” Alisema Asha.

Pia aliongeza kuwa ni vyema kila mmoja wetu kutumia ushauri tulioupata kutoka kwa wazazi wetu ambao wametupatia.

MWISHO

Post a Comment

0 Comments