Na Shushu Joel,Kibaha
MWENYEKITI
wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania ( UWT) Mkoa wa Pwani Bi, Zaynab Matitu Vulu
amewataka wana chama wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) kuendeleza umoja na Mshikamano
ili kuweza kuwa wamoja kama ilivyokuwa kwa waasisi wa chama hicho ili kuhakikisha wanashinda kwa kishindo uchaguzi wa serikali za mitaa2024.
Rai hiyo ameitoa alipokuwa akizungumza na wajumbe wa Baraza la UWT Wilaya ya Kibaha Mjini ambapo amesema kuwa panapokuwepo na umoja na mshikamano ushindi ni lazima.

Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Pwani Bi, Zaynab Matitu Vulu akisisitiza jambo mbele ya wajumbe katika moja ya vikao vyake( NA SHUSHU JOEL)
“ Ni muhimu
kuwa wamoja ndipo tutaweza kufanikiwa kwa mahitaji yetu hivyo niwaombe kila
mmoja kwa nafasi yake kuweza kumpenda mwenzake ili kujenga mshikamano” Alisema
Vulu.
Aidha
alisema kuwa kama hakuna umoja na mshikamano changamoto zitakuwa nyingi hivyo
waendelee kushikamana lengo likiwa ni kushinda uchaguzi huo na kwamba pasipo
kuwa na nyenzo hizo ushindi hautopatikana.
Alisema kuwa
kulingana na ratiba ya Taifa kuna uchaguzi mkuu katika ngazi za serikali za
mitaa hivyo ni muhimu kuweza kuwa na Umoja, mshikamano na upendo kitu ambacho
kitatusaidia kushinda kwa kiwango cha hali ya juu.
Akisoma taarifa fupi kwa Mwenyekiti huyo wa Mkoa Katibu UWT wa wilaya hiyo Bi, Mariam Mugasha amemsifu mwenyekiti huyo kwa jinsi ambavyo amekuwa akisisitiza uwepo wa umoja, Upendo na mshikamano kwa wana CCM.

Wajumbe wakimsikiliza Mwenyekiti wao
Aidha
aliongeza Katibu alisema kuwa atahakikisha maelekezo ya Mwenyekiti wa UWT Mkoa
yanafuata na kufanyiwa kazi ili kuweza kuongeza asilimia ya ushindi kwa chama
chetu.
MWISHO
0 Comments