DKT BITEKO ANAVYOITAFASIRI KAULI YA KNK KWA VITENDO

Na Shushu Joel,Bukombe

MBUNGE wa Jimbo la Bukombe  Mkoani Geita ambaye pia ni Waziri wa Nishati na Waziri Mkuu Dkt Dotto Biteko amezidi kuwana kinara wa kutafasiri kauli mbiu ya wananchi wa jimbo hilo ya kusema na kutenda (KNK) kwa vitendo Zaidi

Naibu Waziri Mkuu Dkt Dotto Biteko akifafanua jambo

Wakizungumza kwa wakati tofauti tofauti wananchi wa jimbo hilo wamempongeza Dkt Biteko kwa kufanikiwa kwa asilimia kubwa kwa uwakilishi wake wa wananchi katika Bunge la Jmahuri la Muungano wa Tanzania.


Amina Hamis(46) ni mkazi wa kata ya Uyovu mara baada ya kuzungumza na waandishi wa habari alisema kuwa Jimbo la Bukombe limepiga hatua kubwa katika maendeleo hii ni kutokana na uongozi bora unaoonyeshwa na Mwakilishi *Mbunge Dkt Biteko) kwani amefanikiwa kutuvusha wananchi wake.


Aidha alisema kuwa hata uchumi wa wakazi wa Bukombe umekuwa sana na hii ni kutokana na uwepo wa miundombinu ya barabara ya uhakika na yenye kupitikana wakati wote hivyo usafirishaji wa mazao umekuwepo kwa wakati na kupelekea wananchi kupata fedha.


Naye Juma Manamba(67) amesema kuwa Dkt Biteko amefanikiwa kututimizia mahitaji yetu wananchi wa Bukombe kwani kile ambacho tulikuwa tukikihitaji kimefanyika kwa vitendo.


Aliongeza kuwa mengi yametendeka katika jimbo la Bukombe chini ya Dkt Biteko yote haya yanatokana na upendo wake mkubwa kwa jamii ndio maana maendeleo yanazidi kufanyika kwa haraka sana’

MWISHO

Post a Comment

0 Comments