Na Shushu Joel,Bukombe
JUMUIYA ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Geita ( UVCCM) umeapa kumlinda kwa hali na mali Mbunge wa Jimbo la Bukombe ambaye pia ni Waziri wa Nishati ambaye pia ni Naibu Waziri Mkuu Mhe. Dotto Mashaka Biteko kuwa utaendelea kumlinda kutokana na kuwa Dkt Biteko ni Mboni ya jicho katika Mkoa wa Geita.
Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Geita akifafanua jambo mbele ya wajumbe wa baraza la umoja huo(NA SHUSHU JOEL)
Akizungumza
mara baada ya kikao cha Baraza la jumuiya hiyo Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Geita Manjale Magambo alisema
kuwa Rais wa Jamhuri wa Tanzania Dkt
Samia Suluhu Hassan ametuheshimisha sana wananchi wa Mkoa wa Geita kwa kumteua
Mhe. Dkt Dotto Mashaka Bitekonkuwa Naibu Waziri Mkuu hivyo ni zamu yetu
kuhakikisha Dkt Biteko analindwa kama mboni ya macho zetu.
Aidha
aliongeza kuwa Biteko amekuwa ni kiongozi wa pekee na wa kuigwa katika Taifa
letu kwani amekuwa msimamizi na mtendaji mzuri katika kuhakikisha maendeleo ya
wananchi yanapatikana kwa haraka ili kuondoa changamoto zinazowakabili.
Hivyo amemtaka Dkt Biteko kupiga kazi bila wasiwasi ya aina yeyote ile kwani Umoja wa Vijana tumeamua kumlinda ili atuletee maendeleo sisi wananchi wa Bukombe na Geita kwa ujumla.
Naye Mjumbe
wa baraza hilo ambaye pia ni Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Bukombe Nelvin
Salabaga alisema kuwa Dkt Biteko amekuwa ni kiongozi wa maendeleo na sio
kiongozi wa maneno maneno hivyo Vijana wa Bukombe tunamatumaini m,akubwa ya
kuendelea kupata maendeleo kutoka kwa Mbunge wetu Biteko.
Aidha
amempongeza Dkt Biteko kwa ufanisi wa ujenzi wa ofisi ya CCM ya Wilaya ambayo
sasa inazidi kuipa heshima Bukombe
MWISHO
0 Comments