Na Shushu Joel,Bukombe
MGANGA Mkuu wa hospitali ya Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita Dr. Deograsia Mkapa amewapongeza wananchi wa wilaya hiyo kwa jinsi ambavyo wamekuwa mstali wa mbele katika kuitikia wito wa kupeleka watoto kupata chanjo ya Meascles Rubella
Mganga Mkuu wa Bukombe Dr, Mkapa akimshika mtoto ili aweze kupatiwa chanjo( NA SHUSHU JOEL)
Akizungumza
na baadhi ya wanawake waliojitokeza kuwaleta watoto kupata chanjo hiyo Dr Mkapa
alisema kuwa zoezi hilo lina siku tatu sasa tangu kuzindiliwa kwake na Mkuu wa
wilaya hiyo Ndugu Said Nkumba lakini
limezidi kuwa na mafanikio makubwa na
yenye tija kwa ujumla
Aidha
amewashukuru wananchi wa Bukombe kwa jinsi ambavyo wamekuwa wakijitokeza kwa
mazoezi ya chanjo mara tu serikali inapowatangazia uwepo wa zoezi hilo.
Pia Dr Mkapa amemsifu Rais wa Jamhuri a Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kujali wananchi wake kwa asilimia mia ndio maana chanjo hizi zinatolewa bure kwa wananchi kweli huyu ni kiongozi wa pekee.
Naye Bi,
Mwanahawa Ally amempongeza Mganga Mkuu Dr, Mkapa kwa kuwa mstali wa mbele
katika kutoa na kusimamia huduma bora katika wilaya ya Bukombe Hivyo Dr Mkapa
amezidi kuwa mfano wa kuigwa kwa watoa huduma jambo ambalo limekuwa likipelekea
huduma kuzidi kuwa bora kila kunapokucha katika wilaya ya Bukombe.
MWISHO
0 Comments