Na Shushu Joel,Bukombe
MKURUGENZI Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Bukombe Mkoani Geita Ndugu George Lutendano amefungua milango ya uwekezaji kwa makampuni,Taasisi na watu binafsi kuweza kujitokeza kuwekeza katika wilaya hiyo kwani inauhitaji wa wawekezaji katika Nyanja mbalimbali.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Bukombe George Lutengano
Rai hiyo
ameitoa alipokuwa ofisini kwake hivi karibu ambapo amesisitiza kuwa wilaya ya
Bukombe ina kila aina ya raslimali zenye kuwafanya kuweza kuja kuwekeza katika
wilaya ya Bukombe.
Alisema kuwa
Wilaya ya Bukombe imezungukwa na madini mengi sana hivyo ni wakati wa mashirika
mbalimbali kuweza kujitokeza kwa wingi ili kuja kuwekeza katika uchimbaji wa
madini, kilimo cha mazao ya chakula na yale
ya Biashara na pia katika ufugaji wa mifugo ya aina yote kwani malisho yapo na
yenye uhakika.
Aidha
Mkurugenzi Lutengano amewata wananchi wa Bukombe ambao wanaishia nje na Bukombe
kutumia pia mahusiano yao kuweza kuwashawishi marafiki zao kuweza kuja na
kuwekeza Bukombe na hata wao ni wakati wao sasa kuwekeza nyumbani kwao ili
kubadilisha mazingira.
“Bukombe ya
sasa sio ile ya miaka ya nyuma kwani sasa hivi kuna miundombinu ya uhakika na
yenye kuvutioa kwa wawekezaji” Alisema Lutengano.
Kwa upande
wake Michael Ally mmoja wa wawekezaji wa
mifugo Wilayani humo amewataka wawekezaji kuja Bukombe kwani kuna Amani kubwa na nafasi za kutosha katika
Nyanja ya uwekezaji.
Aidha
aliongeza kuwa Bukombe kuna kila aina ya uwekezaji kikubwa ni ubunifu tu wa
nini kifanyike na kufuata utaratibu wa uwekezaji kwa serikali yetu
MWISHO
0 Comments