Na Shushu Joel,Temeke
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Temeke JIjini Dar es Salaam Ndugu Khamis Slim ameongoza zoezi la upandaji wa miti Zaidi ya elfu moja katika kata ya Chamanzi ili kuweza kusaidia kuongeza uoto wa asili ambao umekuwa ukipotea kutokana na shughuli mbalimbali ambazo zimekuwa zikifanywa na binadamu kila kukicha.
Akizungumza mara baada ya shughuli za upandaji wa miti hiyo Mwenyekiti Slim alisema kuwa wameamua kufanya hivyo ili kuongeza chachu kwa wananchi kuweza kutambua thamani ya uoto wa asili pia kutokomeza maporomoko ya maji jambo ambalo limekuwa likiongeza kila kukicha kutokana na ukatikaji miti ovyo.
Aidha aliwataka viongozi wa Chama na serikali
kuhakikisha wanaitunza miti hiyo ili iweze kuwa na tija kubwa katika jamii
kwani mpaka sasa hakuna mwananchi ambaye hajaona madhara ambayo yamekuwa
yanafanywa na maji hasa wale wanaoishi mabondeni na sehemu ambazo zimeathirika
na ukataji miti ovyo.
“Niwapongeze sana wananchi wa mtaa wa Mwembe bamia
ambao mmejitokeza kwa wingi kushiriki kwenye zoezi la upandaji miti na ni
ishara tosha kuwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan anakubalika katika wilaya ya
Temeke” Alisema Mwenyekiti Slim
Kwa upande wake Diwani wa kata hiyo John Gama amempongeza Mwenyekiti huyo kwa kuona umuhimu mkubwa na kuwaletea wakazi wa mtaa wa Mwembe Bamia miti hiyo ili kuweza kupandwa kwenye eneo la pembeni mwa barabara.
Aidha aliongeza kuwa ni jukumu letu wananchi
kuhakikisha tunaenzi michango mikubwa ya kimaendeleo ambayo inafanywa na
viongozi wa chama na serikali katika
kata yetu ya chamanzi.
Diwani huyo aliongeza kuwa miti hiyo inaenda kuwa
kielelezo kikubwa kwa wananchi wa chamanzi pia ni vyema nasi kuendeleza kupanda
miti hata mitatau kwenye kila kaya zili kuunga mkono juhudi za Mwenyekiti Slim
MWISHO
0 Comments