MKUU wa wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani Zainabu Kawawa ameitaka mamlaka ya Bandari nchini(TPA) kumuondoa mtumishi ambaye amekuwa ni kero kwa wafanyabiashara katika wilaya hiyo.
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Zainabu Kawawa akifafanua jambo mbele ya wafanyabiashaara wa bandarini(PICHA NA SHUSHU JOEL) |
Aliongeza kuwa awali serikali ya wilaya ilikuwa ikipambana na wimbi la vijana ambao walikimbia kwenye bandari hiyo na kukimbilia mtaani ambako walikuwa wakifanya mambo ya ovyo ingawa serikali iliwachukulia hatua kali za kinidhamu na kuacha tabia hiyo.
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Zainabu Kawawa(SHUSHU JOEL) |
Pia Kawawa aliongeza kuwa amewaomba wafanyakazi hao kuendelea na shughuli zao za kila siku katika eneo hilo kwani mtumishi huyo ni lazima aondoke kutokana na kuwanyanyasa wafanyabiashara kwenye eneo hilo pia kuikosesha wilaya mapato.
Aidha Kawawa amesikitishwa na kitendo kilichofanywa na TAKUKURU kwenda kwenye bandari hiyo na kutaka kuwakamata wafanyabiashara hao kwa kosa la kukwepa kodi kitu ambacho sio sahihi kwao.
Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Zainabu Kawawa akisisitiza jambo |
Kwa upande wake Afisa forodha wa bandari hiyo ya Bagamoyo alisema kuwa wamefanikiwa kukamata madumu ya mafuta ambayo yalikuwa yakikwepeshwa kulipa kodi.
MWISHO
0 Comments