WANACHAMA 35 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Jimbo la Bagamoyo Mkoa wa Pwani, wamejitokeza kuchukua fomu za kuwania ubunge katika jimbo hilo, akiwemo aliyemaliza muda wake Dkt. Shukuru Kawambwa.
![]() |
Aboubakary Mlawa akijaza fomu katika ofisi za ccm huku mbunge aliyemaliza muda wake akishuhudia jambo hilo. |
![]() |
Mbunge aliyemaliza muda wake Dkt. Shukuru Kawambwa akichukua fomu ya kutetea nafasi yake kutoka kwa Katibu wa chama hicho Gertrude Sinyinza. Picha na Omary Mngindo. |
"Wanachama wamehanasika sana na wamejitokeza kwa wingi, kwa siku mbili yaani Julai 14 na 15 saa saba mchana tayari wanachama 50 wameshachukua fomu za kuwania ubunge katika wilaya ya Bagamoyo yenye majimbo ya Chalinze na Bagamoyo," alisema Sinyinza.
Aidha aliongeza kuwa kwakuwa bado siku mbili kabla ya mwisho wa zoezi hilo, anaimani kubwa wana-CCM zaidi wataendelea kujitokeza kuwania nafasi hiyo kwenye majimbo hayo, huku akiwaasa kuwa watulivu katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye kura za maonina uchaguzi hapo Oktoba mwaka huu.
![]() |
Mwana-CCM Saumu Katundu akipokea fomu ya kuwania ubunge jimbo la Chalinze kutoka kwa Katibu wa chama hicho Gertrude Sinyinza. Picha na Omary Mngindo. |
MWISHO
0 Comments