BILAL MUSLIM YAMPIGA JEKI MLEMAVU

Na Omary Mngindo, Bagamoyo

TAASISI ya Bilal Muslimu Mission Julai 12 imemkabidhi baskeli ya miguu mitatu Salum Lila mkazi wa Bagamoyo Mkoa wa Pwani ambaye ana ulemavu wa miguu.


Mwenyekiti wa Bilal Muslim Mission Anwar Melali akimkabidhi Salum Lila baiskeli ya mataili matatu. Picha na Omary Mngindo
Mbali ya utekelezaji huo uliotokana na ombi la Mkuu wa Wilaya Zainab Kawawa, aliyeliwasilishia kwa Mbunge aliyemaliza muda wake Dkt. Shukuru Kawambwa, aliyekutana na viongozi wa taasisi hiyo hatimae kumkabidhi baskeli hiyo.

Katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya, mbali ya viongozi wa taasisi hiyo, Mkuu wa wilaya Zainab Kawawa aliyewakilishwa na Katibu Tawala Kasilda Mgeni, akiwemo Kawambwa ambapo pia walikabidhi matenki madogo 9 na sabuni kwa ajili ya shule tatu ikiwa ni kudhibiti ugonjwa wa Corona.

Anwar Melali akimkabidhi Kasilda Mgeni matenki 9 ya maji yatayokabidhiwa kwenye shule tatu wilayani hapa, anayeshuhudi ni Mbunge aliyemaliza muda wake Dkt. Shukuru Kawambwa. Picha na Omary Mngindo.
Akizungumza katika hafla fupi Kasilda alisema kuwa anawashukuru viongozi wa taasisi hiyo kwa namna wanavyoendelea kuwasaidia wana-Bagamoyo, huku akilpongeza ukaribu wa Bilal na Mbunge anayemaliza muda wake, kwani ndiye aliyewatafuta kwa aajili ya wananchi.

"Pia kuna mahusiano mazuri kati Kawambwa na Kawawa kwani wamekuwa na ukaribu wa kazi mbalimbali, lakini kwaniaba ya Mkuu wa wilaya na wana-Bagamoyo shukrani zaidi nizilete kwenu kwa ukarimu mkubwa kwa wananchi wetu," alisema Kasilda.

Mwenyekiti wa Bilal Muslim Mission Anwar Melali akimkabidhi Salum Lila baiskeli ya mataili matatu. Picha na Omary Mngindo.
Akizungumza kwa niaba ya viongozi wenzake mmoja wa maofisa wa taasisi hiyo Ayn Shariff alisema kuwa kumekuwepo na ushirikiano mkubwa kati yao na Dkt. Kawambwa, huku wakimuombea dua aweze kutetea tena nafasi hiyo ili waweze kuwatumikia zaidi wana-Bagamoyo.

Akitoa shukrani kwa wana-Bilal Muslim, Kawambwa alisema kuwa taasisi hiyo imejitoa kwa kiasi kikubwa katika kuwatumikia wana-Bagamoyo katika sekta mbalimbali, ikiwemo tiba ya macho waliyoitoa miezi michache iliyopita ambapo wakazi zaidi ya 3,000 walipatiwa huduma hiyo pasipomalipo.

Mbunge aliyemaliza muda wake Dkt. Shukuru Kawambwa akimkabidhi Salum Lila baiskeli ya mataili matatu iliyotolewa na taasisi ya Bilal Muslimu Mission, wanaoshuhudia Anwar Melal na Mwenyekiti wa taasisi na Kasilda Mgeni Katibu Tawala. Picha na Omary Mngindo.
"Kwaniaba ya wana-Bagamoyo tunawashukuru sana viongozi wa Bilal kwa namna wanavyojitoa katika kutuaaidia katika nyanja mbalimbali, kwa niaba ya wananchi tunaendelea kuwaombea dua muwe na afya njema muendelee kututafutia wafadhili zaidi wake kutusaidia zaidi," alimalizia Kawambwa.

Kwa upande wake Lila akitoa neno la shukrani kwa Kawambwa, alianza kumshukuru kwa jitihada zake, huku alisema anamuombea dua arejee kwenye nafasi hiyo ili aendelee kiwasaidia wengine wenye mahitaji mbalimbali.

MWISHO

Post a Comment

0 Comments