WANANCHI SIMIYU WAKIRI MTAKA AMEWAFUTA MATONGOTONGO.

Na Shushu Joel,Simiyu.

WANANCHI  mbalimbali wa Mkoa wa Simiyu wanaozidi kujionea maajabu mengi yanayojitokeza kwenye maonyesho ya Nane Nane mkoa humo wamekiri ya kuwa kila jambo linalofanyika mkoa humo chanzo chake ni mkuu wa mkoa wao.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka akizungumza na baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye viwanja vya Nane Nane Nyakabindi(SHUSHU JOEL)
Wakizungumza kwa wakati tofauti tofauti wananchi wa mkoa huo walisema kuwa Mkuu wa Mkoa Anton Mtaka ndiye ameubadilisha mkoa wetu kwa kila jambo la maendeleo na hivyo ametufuta matongotongo wakazi wengi wa mkoa huu.

Nkali Suluja (54) mkazi wa Ngasamo wilaya ya Busega Mkoani humo alisema kuwa maonyesho ya nanenane yamekuwa msaada mkubwa kwa wanasimiyu  kutokana na yale yanayotendeka kwenye Mkoa wetu wa Simiyu kwa juhudi za Mkuu wa Mkoa

Nkali Suluja mwenye kofia akipata maelekezo ya jinsi ya kufuga samaki na kuweza kuondokana na changamoto za maisha kutoka kwa Afisa Mifugo wilaya ya Maswa.
“Kwa kweli Mkuu wa Mkoa Mtaka ametufumbua macho kwa kutuunganisha na mikoa mbalimbali ya jirani pia hata ya mbali nao wamekuwa wakija simiyu kujifunza vitu mbalimbali ikiwemo viwanda na umoja wa wananchi wa mkoa huo”Alisema Suluja.

Aidha aliongeza kuwa miaka ya nyuma mkoa wa simiyu ulikuwa na viongozi wa juu lakini uwepo wa Mtaka umechangia kukua na kuimarika kwa mkoa wetu ikiwemo viwanda,kukua kwa elimu kuimarika kwa ulinzi na usalama ndani ya mkoa wetu.

Moja wa Ng'ombe wa kisasa waliopo kwenye maonyesho ya Nane Nane Simiyu.
Hivyo tunaiomba serikali kupitia vyombo vya habari kutusaidia kuendelea kuwepo kwa maonyesha haya ya Nane Nane kitaifa kwenye mkoa wetu kwani wananchi wengi sasa wanazidi kuamka na kujua umuhimu wake kwa kuchangamkia fursa mbalimbali za mafunzo pia kujionea teknologia nyingi tokea sehemu mbalimbali.

Kwa upande wake Tabitha Masanja aliyefika kwenye maonyesho ya Nane Nane kwenye viwanja vya Nyakabindi kwa mara ya kwanza anasema kuwa kwa kweli nimejionea mambo mengi mazuri ambayo nilikuwa sijawai kuona kwenye maisha yangu kutokana na kuwa maonyesha yalikuwa yakifanyika mbali na makazi yetu.

Aliongeza kuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anton Mtaka amekuwa nguzo kubwa kwa wakazi wa Simiyu kutokana na upambanaji wake wa kazi kwa kuwafungulia  fursa nyingi wakazi wa Mkoa uo kwa ujumla

Bi Tabitha Masanja mwenye mtoto kushoto akiangalia jinsi ya kufuga samaki kwa njia ya kisasa
Hivyo ameiomba serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt John Pombe Magufuli kuendelea kuamini mkoa wa Simiyu ili uendelee kutumia viwanja hivi kuwa ndio sehemu ya maonyesho ya Nane Nane kwa kipindi chote kitaifa ili wakazi waendelee kufumbua macho yao kama ilivyo sasa.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anton Mtaka alipohojiwa na mwandishi wa habari alisema kuwa yeye ni mtendaji wa serikali hivyo ni wajibu wake kuhakikisha wananchi wa mkoa wake wanapata fursa za kutosha kutoka serikalini na kwa wadau mbalimbali .

 

Aidha aliongeza kuwa yeye peke yake asingeweza kufanya jambo lolote lile bali ni ushirikiano mkubwa anaoupata kutoka kwa wasaidizi wake pamoja na wananchi ambao wamekuwa msaada mkubwa kwa kuhakikisha Simiyu inasonga mbele kwenye maendeleo.

Baadhi ya wananchi waliojitokeza kujionea jinsi gani unaweza kufuga samaki kwa njia ya kisasa na kuweza kujipatia kipato
Pia Mtaka amewataka wananchi kuendelea kujitokeza kwenye viwanja hivyo ili kujizolea elimu kutoka taasisi mbalimbali zilizopo kwenye maonyesho hayo.

“Kauli mbiu ya Nane Nane kwa mwaka huu iko wazi na inasema kuwa kwa Maendeleo ya Kilimo na Uvuvi Chagua Viongozi Bora 2020”

MWISHO

 

 

 

Post a Comment

0 Comments