SEKTA YA AFYA YAZIDI KUPAA SIMIYU

 

 

 Na Anita Balingilaki, Bariadi

Kutoka kulia ni mganga mkuu wa mkoa wa Simiyu Festo Dugange katika ni naibu waziri wa wizara ya afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Godwin Mollel na kushoto ni mganga mfawidhi wa hospitality ya rufaa ya mkoa wa Simiyu Matoke Muyenjwa(ANITA BALINGILAKI)

 Naibu waziri wa afya ,maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Dkt Godwin Mollel kupitia wizara ya afya, amesema wizara  imejipanga kuunganisha hospitali ya rufaa ya mkoa wa Simiyu na hospitali ya muhimbili kwa lengo la kuwarahisishia wagonjwa kupata  matibabu kwa urahisi.

Muonekano wa majengo ya hospitali ya rufaa ya mkoa wa Simiyu

Hayo yamebainishwa mapema Aug 7 na naibu waziri hiyo mara baada ya kutembelea ujenzi wa mradi wa jengo la mama na mtoto katika hospitali ya hiyo iliyopo Nyaumata mjini Bariadi.

Amesema kuwa kabla ya kuwepo kwa hospitali hiyo wagonjwa walikuwa wakilazimika kwenda nje ya mkoa ikiwemo Bugando ya jijini Mwanza kutibiwa ambapo kwa sasa wanapata huduma kwa urahisi ndani ya mkoa.


Awali mganga mkuu wa mkoa wa Simiyu Dkt Festo Dugange ameeleza kuwa kwa kipindi cha miaka 5 ya serikali ya Dkt John Pombe Magufuli kumewepo na ongezeko la vituo vya afya kwa zaidi ya 40% kutoka 196 hadi kufikia 218 ambavyo vimepunguza tatizo la vifo vya kinamama na watoto wachanga

Muonekano wa hospital ya mkoa wa Simiyu mara baada ya kukamilika
 

Kwa upande wake mganga mfawidhi wa hospitali hiyo hospitali  Dkt Matoke  Muyenjwa ameongeza wametenga kiasi cha shilingi milioni 300  kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba.


MWISHO

Post a Comment

0 Comments