WANANCHI SIMIYU KUNEEMEKA NA HUDUMA YA MAJI SAFI NA SALAMA.

Na Anita Balingilaki, Simiyu

Upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama mkoani Simiyu  unatarajiwa kuongezeka kutoka  asilimia  51%   mwaka 2019  hadi  57.4 %  ifikapo 0ctoba 2020 kupitia mradi wa Programu  kwa matokeo ya (PF4R ) hali itakayosaidia wananchi kupata  huduma hiyo kwa uhakika na urahisi.

Mbali na ongezeko hilo pia kutakuwepo na ongezeko la ajira kwa wananchi ambao watajipatia  kazi kupitia mradi wa usambazazji  wa mabomba katika miradi 23 itakayotekelezwa.

ushoto ni meneja wa wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini ( RUWASA) mhandisi Mariam Majala akionesha mabomba yatakayotumika kwenye  utekelezaji kulia ni katibu tawala mkoa wa Simiyu Mariam Mmbaga(NA ANITABALINGILAKI)

 Hayo yamesemwa leo na meneja wa wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA) mhandisi Mariam Majala wakati wa makabidhiano ya mabomba yatakayotumika kutekeleza miradi ya mji mkoani humo yaliyofanyika katika ofisi za RUWASA mjini Bariadi.

Mhandisi Majala alisema  mpaka sasa wamepokea   70 % ya mabomba ya maji yenye thamani ya milioni 823 ambayo yatatumika kutekeleza miradi 23 kwa mkoa mzima huku wakisubiria wakati wowote kuwasili kwa 30 % ya mabomba  yaliyobaki.

" hali ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa sasa sio mbaya na nawahakikishia wananchi ongezeko kubwa la huduma hiyo" alisema Mhandisi Majala.

eneja wa wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini ( RUWASA) mhandisi Mariam Majala akionesha mabomba


Awali akikagua mabomba haya katibu tawala mkoa wa Simiyu Mariam Mmbaga aliwataka wananchi kushiriki kwenye mradi huo kwa kutunza miundombinu ya maji ili lengo la ongezeko hilo walilokusudia liweze kufikiwa  huku akiipongeza bodi ya manunuzi kwa kazi nzuri iliyofanyika.

" niwatake wananchi wa  mkoa huu ( Simiyu) kuitunza miundombinu ya maji inayotekelezwa na serikali ili iweze kudumu na kuwanufaisha wote kama ilivyokusudiwa"alisema Mmbaga

                    Baadhi ya mabomba yatakayotumika kwenye utekelezaji.

Kwa upande wake mjumbe wa bodi manunuzi Ekwabi Mujungu  ameomba kazi ifanyike kama ilivyopagwa ili thamani ya fedha ionekane .

MWISHO

 

Post a Comment

0 Comments