DC SANGA AWATAKA WALIMU KUTUNZA THAMANI.

Na Shushu Joel,Mkuranga.

MKUU wa Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani Filberto Sanga amewataka walimu wote katika wilaya hiyo kuwa mstali wa mbele katika kutunza thamani za shule ili zitumike kwa muda mrefu.

Mkuu wa wilaya ya Mkuranga Filberto Sanga akizungumza na walimu wa shule ya sekondari Vikindu(NA SHUSHU JOEL)

Rai hiyo ameitoa alipokuwa akizungumza na walimu wa shule ya sekondari Vikindu alipofika shuleni hapo ili kujionea jinsi gani maandalizi ya wanafunzi wa kidato cha kwanza yanavyofanyika kwa upande wa shule.


“Walimu wangu nyie tunawategemea sana kutufundishia watoto wetu ili hapo baadae waje kuwa kama tulivyo sie leo hivyo tuwasisitize watoto wetu wawe waangalifu na mali hizi za serikali”Alisema Sanga

Mkuu wa wilaya Mkuranga Filberto Sanga akikagua majengo ya shule.


Aidha aliongeza kuwa serikali ya wilaya imejipanga kisawasawa juu ya wanafunzi wanaotarajia kuanza shule hivi punde cha msingi ni kuendeleza ushirikiano kuanzia kwa wazazi mpaka serikali ili kuhakikisha zoezi ili linakwenda kama lilivyopangwa.

Aliongeza kuwa Serikali imekuwa ikitumia pesa nyingi ili kuhakikisha miundombinu ya upatikanaji wa elimu kwa wanafunzi inakuwa ni rafiki hivyo kila mmoja anatakiwa kutunza thamani za shule kama wao wanavyothaminiwa na serikali.


Kwa upande wake walimu wa majengo wa shule hiyo Bw, Athumani Ally amemwakikishia mkuu huyo wa wilaya kuwa kipindi hiki hakuna mchezo utakaofanyika na hasa juu ya upotevu au kuvunjika  kwa thamani za shule na kama mwanafunzi atakayebainika kufanya hivyo basi hatua kali za kinidhamu zitachukuliwa juu yake.


Aidha Mwalimu huyo amempongeza mkuu wa wilaya kwa jinsi amekuwa msaada mkubwa kwa sekta ya elimu kwenye wilaya hiyo kwani amekuwa akitembelea mara kwa mara mashuleni na hivyo amekuwa akitupatia moyo wa dhati walimu.

Naye Mmoja wa wazazi waliokuwa wamejitokeza shuleni hapo kuangali watoto wao wamemsifu mkuu huyo wa wilaya kwa jinsi anavyopambania kukua kwa elimu kwenye wilaya ya Mkuranga.

MWISHO

Post a Comment

0 Comments