KIKWETE ATEULIWA

 Na Shushu Joel


Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mkoani Pwani Mhe Ridhiwani Kikwete ameteuliwa kuwa mjumbe wa kamati ya kudumu ya Kanuni za Bunge na kwenye kamati ya sheria ndogo ndogo.


Kwa uteuzi huo,  Mbunge Kikwete  atakuwa na majukumu yakusimamia Kanuni, kurekebisha na kufafanua kanuni na sheria zilizogatuliwa kisheria. 


Wabunge wapo Dodoma kwa ajili ya vikao vya Kamati vinavyotarajiwa kuanza leo ambapo  watapewa mafunzo kabla ya kuanza utekelezaji wa majukumu yao katika Mkutano wa  pili wa Bunge la kumi na mbili lilipangwa kuanza 02,February 2021.


Imetolewa na:

Kitengo cha Habari

Ofisi ya Mbunge 

Jimbo la Chalinze

Post a Comment

0 Comments