WAKAZI SOGA WALILIA MAJI SAFI NA SALAMA.

 Julieth Ngarabali, Kibaha

Wakazi wa Kata ya Soga Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani wamedai wako hatarini kukumbwa na magonjwa ya mlipuko kwakuwa wanalazimika kunywa  maji ya kisima ambayo wamesema kuwa si salama kwa Matumizi ya binadamu kulingana na mazingira yalivyo.

Mtendaji mkuu was DAWASA Cyprian Luhemeja (kushoto) akitoa maelezo juu ya hatua mbalimbali zinavyofanyika na kituo cha kusambaza maji Mlandizi Kibaha mkoan Pwani kabla ya kuwafikia wateja , kulia ni Mbunge wa Kibaha vijijini Michael Mwakamo.


Hayo yamebainishwa na wakazi hao kwenye ziara ya mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini Mkoani Pwani Michael Mwakamo alipofika Kwenye Kata hiyo   kwa lengo la kusikiliza changamoto zinazowakabili wakazi hao ambaye awali alitembelea Kituo cha DAWASA  Mlandizi Ili kujionea hatua mbalimbali za usambazaji maji kwa wateja.


Kwa mujibu wa wakazi hao  walidai  kuwa tayari wameshaanza kupata madharambalimbali  kiafya kwa kuugua homa za matumbo taifodi huku wakiamini kuwa chanzo cha kupata matatizo hayo ni maji wanayotumia.


"Mpaka sasa ni zaidi ya mwezi mmoja umepita  mabomba ya DAWASA hayatoi maji lakini hatujui Sababu ni nini hivyo tunalazimika kunywa maji ya kisima ambayo kimsingi si Salma lakini tunalazimika kufanya hivyo kwakuwa tumekosa maji safi ya kunywa"alisema. Pili Mgaya


Kwa upande wake Fatima Saidi alisema kuwa tangu alipoanza kutumia maji hayo amekuwa akisumbuliwa na kuumwa tumbo hali ambayo kimsingi inamuathiri kiafaya na kiuchumi kwani amekuwa akitumia sehemu ya pesa zake kwaajili ya dawa na kuomba Mamlaka zinazohusika kufanya jitihada za kurejesha huduma hiyo Ili kuwaondolea adha wanayoipata.


Awali Mtendaji  Mkuu wa DAWASA Cyprian Luhemeja akielezea mikakati ya kuboresha huduma ya maji kwa wakazi wa Wilaya ya Kibaha alisema kuwa hadi kufikia mwezi Desemba mwaka huu maeneo yote ya Mlandizi yatakuwa na huduma ya maji wakati wote.


Alisema kuwa ujenzi wa miradi ya maji unaendelea kutekelezwa  kwa wakati hivyo maeneo yote yaliyokuwa na changamoto ya huduma ya maji hali hiyo haitajitokeza baada ya mwezi huo wa Desemba bali Wananchi wote wataendelea kupata huduma hiyo muhimu kwa uhakika.


"Tunaleta mabomba kwa wingi na Vijana watakaofanyakazi hiyo ni wa hapa maeneo ya jirani hivyo nieaombe wajiandae na shughuli ya kuchimba mitaro ya kusambaza mabomba ya maji"aliaema


Akizungumzia hali hiyo Mbunge wa Jimbo hilo Michael Mwakamo alisema kuwa ataenda kushauriana na watumishi wa DAWASA Ili kufanya jitihada za kurejesha huduma ya maji kwenye Kijiji hicho.


Mwiaho

Post a Comment

0 Comments