MBUNGE SONGE AWATAKA WANANCHI KUJITOKEZA KWA WINGI KUPATA CHANJO YA CORONA.

Na Shushu Joel,Busega

MBUNGE wa jimbo la Busega Mkoani Simiyu Simon Songe amewataka wananchi wa jimbo hilo kila mmoja kwa wakati wake  kuhakikisha anakwenda kupata chanjo ya covid 19.

Mbunge wa Jimbo la Busega Mhe:Simon Songe akiwashuudia vijana wakipata chanjo siku ya fainali ya SONGE CUP(NA SHUSHU JOEL)

Akizungumza na wananchi mbalimbali waliojitokeza kwenye fainali ya mashindano ya SONGE CUP yaliyozikutanisha timu za kata ya Kiloleli na Shigala Mbunge huyo alisema kuwa unapopata chanjo ya Corona unaepukana na mambo mengi hivyo ni jukumu la kila mmoja wetu kuchangamkia fursa hiyo ya chanjo inayotolewa na serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan bila malipo.

Aidha alisema kuwa kuna watu wamekuwa wakipotosha juu ya chanjo hii ya Covid 19 nawaombeni wananchi wenzangu watu wa namna hiyo ni bora mkawapuuza kabisa kwani chanjoi hizo hazina madhara ya aina yeyote ile katika mwili wa binadamu  kwani ni salama kwa Afya zetu.

“kila mmoja wetu amemuona kiongozi wetu,Mama yetu Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amekuwa wa mfano kwa kupata chanjo na pia ametuhakikishia chanjo hizo ni salama salimini hivyo niwaombe twende tukachanje”Alisema Songe

Aidha Mbunge huyo aliwashauri wataalamu wa Afya kuendelea kutoa elimu kwa jamii kwani wananchi wako tayari kupata chanjo lakini tatizo limekuwa ni kufikiwa kwao hivyo ni vyema tukatengeneza utaratibu wa kutoa elimu kila panapokucha iwe nyumba kwa nyumba au namna nyingine yeyote ile itakavyokuwa.

Kwa upande wake kiongozi wa timu ya Kiloleli FC Christopher Vincent amempongeza mbunge huyo kwa namna jinsi alivyojipanga katika mashindano hayo kwani yamekuwa ni ya pekee kutoknana jinsi yalivyoandaliwa kuanzia huduma ya utoaji wa elimu ya Covid 19 na mambo mengi mengi.

Aliongeza kuwa kutokana na elimu tuliyoipata  kutoka kwa wataalamu wa Afya imetujengea uwezo mkubwa na uelewa wa hali ya juu kuhusu umuhimu wa chanjo ya Covid 19.

“Tumekuwa washindi wa SONGE CUP leo katika Nyanja mbili ambazo ni kombe pamoja na  elimu yay a chanjo ya corona kweli Mbunge wetu anastahili pongezi sana”Alisema Vincent.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa wilaya ya Busega Godfrey Mbagali amempongeza Mbunge kwa jinsi ambavyo amekuwa msaada mkubwa katika sekta ya Afya kwani kila anapokwenda ajenda yake amekuwa akiwataka wananchi wenye nafasi ni bora wakapata chanjo ya Covid 19 ni salama na ndio maana hata Rais wetu amekuwa wa kwanza kupata kinga ya ungonjwa huo.

Aidha Mbagali amewatoa hofu wananchi kuwa hakuna tatizo lolote lile kuhusu chanjo kwani iko vizuri na hakuna madhara yeyote yale yatokanayo na chanjo hiyo.

MWISHO

 

Post a Comment

0 Comments