“NAUMIA SANA KUONA MWANANCHI MKOA WA PWANI NI MASIKINI" RC KUNENGE.

 Na Shushu Joel Bagamoyo.

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amezidi kusononeshwa na  wananchi wa Mkoa huo kuendelea kuwa masikini huku Mkoa wa Pwani ukiwa na kila Raslimali ya kuwafanya wakazi wa Mkoa huo kuweza kuwa matajiri.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akisisitiza jambo kwa wananchi wa wilaya ya Bagamoyo(NA SHUSHU JOEL)

Akizungumza na wananchi wa wilaya ya Bagamoyo Kunenge alisema kuwa Mkoa wa  Pwani umejaaliwa kuwa na kila kitu ambacho kitamfanya mkazi wa eneo fulani kuwa ni mtu mwenye kipato cha kutosha kwa kupitia raslmali zinzomzunguka mkazi huyo.

 

"Pwani kuna kokoto bora za kutengeneza mabarabara, vituo vya utalii,Ardhi yenye rutuba, viwanda, Bwawa la Mwalimu Nyerere  na vingine vingi vipo kwenye Mkoa wetu kwanini tunakuwa masikini "Alisema  Kunenge.

 

Hivyo Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wananchi wote wa Mkoa huo kuhakikisha wanachangamkia fursa zilizopo ndani ya Mkoa kwa kujiongezea kipato zaidi.

 

Aidha aliongeza Mkoa huu una vitu ambavyo uwezi kuvipata sehemu yeyote ile kwa mfano Makumbusho ya Bagamoyo,Bahari ya blue huko Mafia hivi vyote ni fedha sema ni ubunifu tu wa jinsi gani unaweza kuivuna pesa hizo.

Kwa upande wake Haji Juma mkazi wa kata ya Nia Njema amempongeza mkuu wa mkoa kwa ziara yake ya kata kwa kata katika wilaya ya Bagamoyo huku akisisitiza ni kweli wananchi wa mkoa huu kuwa masikini ni kujitakia tu.

Aidha aliongeza kuwa ni halali Mkuu wa Mkoa wetu Kunenge asononeshe na umasikini wetu huku Mkoa wetu ukiwa na Raslimali nyingi na za kutosha za kumfanya mwananchi kuweza kuwa na uwezo mkubwa wa kipato.

“Elimu ya Mkuu wa Mkoa ni funzo kwetu hivyo wananchi wenzangu tujifunze kupitia maneno ya Mkuu wetu wa Mkoa kwani ni siku chache tu tangu kuwa kiongozi lakini kaona jinsi gani wana Pwani tunavyoshindwa kutumia fursa”Alisema Haji.

Naye Mwanaisha Mwalami amemsifu Mkuu wa Mkoa kwa kuwavuta masikio na kusema kuwa kweli Kunenge ni kiongozi wa maono ya mbali sana.

Pia amewataka wanawake wote Mkoa huo kuyadadafua au kuyatafakali maneno hayo mazito ya Mkuu wa Mkoa juu ya uwepo wa wingi wa raslimali kwenye Mkoa wetu cha ajabu wananchi wake ni masikini kweli inauma.

MWISHO

Post a Comment

0 Comments