RC: KUNENGE AWA MBOGO UCHELEWESHWAJI SOKO LA SAMAKI.

Na Shushu Joel,Bagamoyo

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amemtaka mkandarasi anayejenga soko la samaki katika wilaya ya Bagamoyo Mkoani humo kuhakikisha anakamilisha ujenzi huo ndani ya mkataba kama walivyokubaliana.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akisisitiza jambo kwa mshauri wa mradi (NA SHUSHU JOEL)

Akitoa maagizo hiyo Kunenge alisema ni lazima soko hili likamilike kwa wakati kama ilivyokuwa imekusudiwa na serikali ili wananchi wa hapa waanze kunufaika na serikali yao ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan.

“Naagiza ujenzi wa hapa uwe usiku na mchana kwani siku zilizobaki ni chache sana na wananchi wanahitaji waanze kutumia soko hili kwa wakati”Alisema Kunenge.

Aidha aliongeza kuwa wananchi wa Bagamoyo asilimia kubwa wanategemea bahari kuendesha shughuli zao za kila siku kwani wengine ni wavuvi na wengine ni wasafirishaji hivyo nahitaji soko hili likamilike kwa haraka ili wananchi hawa waanze kujiingizia kipato kutokana na sughuli zao za bahari.

 

“Soko hili linatakiwa kukabidhiwa mwezi wa kumi kwenye tarehe za mwanzo hivyo na nataka tarehe usika soko hilo liweze kukabidhiwa kama ilivyokubaliana la sivyo nitawashitaki kwa kuchelewesha huduma muhimu ya wananchi wangu”Alisema Kunenge.

Muonekano wa soko la samaki wilayani Bagamoyo ulivyo sasa (NA SHUSHU JOEL)

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM wialaya ya Bagamoyo Sharifu Zahoro amempongeza mkuu huyo wa Mkoa kwa jinsi alivyotoa maamuzi ya kukamilishwa kwa soko hilo la samaki ili wananchi wa Bagamoyo waweze kunufaika kwa haraka pia halmashauri kuweza kujiongezea kipato”Alisema Zahoro

Aidha alisema kuwa wao kama upande wa chama ni furaha kubwa kwao kukamilika kwa miradi kya wananchi kwani pindi wanapoenda kwa wananchi wanakuwa nayo ya kujivunia kama chama.


Naye Ally Mbarouk mkazi na mvuvi wilaya ya Bagamoyo alisema kuwa wao kama wavuvi wamefurahi kumuona mkuu wa Mkoa anafika kwenye soko hilo walilolisubilia kwa kipindi kirefu kwa ajili ya kuhakikisha usalam wa shughuliu zao.

Pia aliongeza kuwa ujio wa kiongozi huo kutapelekea kukamilika kwa haraka kwa soko hilo na hivyo shughuli za uvuvi kuendelea kwa kiwango cha hali ya juu.

MWISHO

 

 

Post a Comment

0 Comments