Na Shushu Joel,Kibaha
MLEZI wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Mkoa wa Pwani ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Philip Isdor Mpango amewataka viongozi na wananchi wa Mkoa wa Pwani kuhakikisha wanamtumia ipasavyo Mkuu wa Mkoa huo Mhe:Abubakar Kunenge kwani ni mtu mwenye uchu wa maendeleo.
Makamu wa Rais wa Jmahuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Philip Mpango akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge(NA SHUSHU JOEL)
Rai hiyo
ameitoa hivi karibuni alipokuwa katika
moja ya vikao vyake vya kuzungumza na viongozi mbalimbali wa CCM alipokuwa
amekwenda kujitambulisha kuwa yeye ndiye mlezi wa Mkoa huo kwa upande wa chama
cha mapinduzi(CCM)
Alisema kuwa
maneno hayo mbele ya wana chama wa chama
cha mapinduzi (CCM) kupitia viongozi wao kuanzia ngazi ya kata mpaka Mkoa
Makamu wa Rais Dkt Mpango alisema kuwa kati ya wakuu wa Mikoa wenye uchu wa
kuona wananchi wake wananufaika ni huyu wenu hapa.
Aidha
alisema kuwa utendaji wa kazi zake ni za kimakini na zenye uhakika kwa jamii
inayomzunguka hivyo niwaombe muwe mnamshirikisha kwa kila jambo hili muweze
kufika mbali zaidi ya hapa mlipo.
“Namjua Mkuu
wenu wa Mkoa Kunenge ndio maana nawaombeni muwezi kumtumia katika Nyanja
mbalimbali za kukuza uchumi wa mkoa wetu kwani ni mtu mwenye maono ya
mbali”Alisema Dkt Mpango.
Kwa upande
wake Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi(CCM) wilaya ya Bagamoyo Sharifu Zahoro
amempongeza mkuu wa Mkoa kwa jinsi ambavyo viongozi wakubwa wan chi yetu
wanavyotambua utendaji wake wa kazi katika Mkoa wa Pwani.
Aliongeza
kuwa ni jambo la kumpongeza Rais wetu wa Jmhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Samia
Suluhu Hassan kwa kutusaidia wananchi wa Mkoa wa Pwani kwa kuona jinsi gani
tunahitaji Mkuu wa Mkoa mwenye hekima busara na uadilifu mkubwa na ulio
tukuka kwa wananchi wake na hasa
wanyonge.
Aidha
alisema kuwa wananchi wa Mkoa wa Pwani tuna matumaini makubwa kwa kuona Mkoa wa
Pwani unakua kiuchumi,kisayansi na kisiasa kutokana na uwepo wa kiongozi makini
mwenye kusikiliza changamoto za wakazi wa Pwani na kisha kuzitatua.
“Kwa sasa
Mkuu wetu wa Mkoa Ndugu Kunenge yupo kwenye ziara ya kusikiliza kero za
wananchi ambapo anakwenda kata kwa kata jambo ambalo hapao awali halikuwepo
lakini sasa wananchi wanapatiwa fursa ya kusema kile kinachowakabili na hata
kutoa ushauri jinsi gani Mkoa ufanye ili kukuza uchumi kwa kujenga miundombinu
mbalimbali” Alisema Sharifu.
Naye
Bi,Mwajuma Ally amesifu juhudi za Mkuu huyo wa Mkoa kwa namna jinsi ambavyo
amekuwa akipambana na jinsi gani Mkoa wa Pwani unaweza kupiga hatua kwenye
masuala mbalimbali ya kimaendelea .
Hivyo kwa
niaba ya wanawake tunampongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kumleta Kunenge
katika Mkoa wa Pwani kwa kusudi la kukuza maendeleo kwa wananchi wote kwani
Mkoa huu una kila sababu ya kuwa juu kimaendeleo kutokana na jiografia ya
maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Pwani.
Aidha
alisema kuwa tangu uwepo wa Mkuu wa Mkoa Kunenge kuwepo kwenye Mkoa wetu
manufaa makubwa yameanza kuonekana kwa watu mmoja mmoja na kuongezeka kwa
uwekezaji wa viwanda hizi zote ni juhudi binafsi .
MWISHO
0 Comments