“WAZAZI WASIMAMIENI WATOTO SHULE”RC KUNENGE

Na Shushu Joel,Pwani

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amewakumbusha wazazi na walezi wote katika Mkoa wa Pwani kuhakikisha wanakuwa wasimamizi wakuu wa wanafunzi pindi wanapokuwa majumnbani na pindi wanapotoka shuleni kwa kusudi la kujua maendeleo yao kielimu.

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akifafanua jambo kuhusu umuhimu wa kupeleka watoto shule mbele ya wazazi(NA SHUSHU JOEL)

Akizungumza ofisini kwake Kunenge alisema kuwa wazazi na walezi walio wengi wamekuwa na kasumba ya kutokufuatilia chochote kile iwe nyumbani wala shuleni kinachofanywa na watoto wao hivyo hali hii ni hatari sana kwa kizazi cha kesho.

“Mzazi au Mlezi ni wajibu wako kujua nini alichokifanya mtoto wako pindi anapokuwa shuleni na hata anapokuwa nyumbani itamsaidia sana mwanafunzi kumjengea uwezo wa kifkra mara kwa mara na kuwa mwepesi kuweza kuyakumbuka yale wanayoelekezwa shuleni” Alisema Kunenge.

Aliongeza kuwa ushirikiano baina ya wazazi,walezi na walimu utatengenezwa kizazi chenye uwezo mkubwa katika Mkoa wetu na hivyo kuwa na vijana wengi watakao ongeza nguvu kubwa katika serikali yetu kwa kipindi kijacho.

Aidha Kunenge alisema kuwa serikali ya awamu ya sita imewekeza fedha nyingi katika miundombinu ya elimu kwenye Mkoa wa Pwani hivyo sasa Wazazi na walezi ni jukumu lao kuisaidia serikali kuhakikisha wanawasimamia wanafunzi ili kuweza kuwa na kizazi cha wasomi ambao watakaokuja kuja lulu kubwa katika Mkoa wetu wa Pwani.

Mbunge wa kibiti kushoto na mbunge wa Bagamoyo wakimfutialia kwa makini mkuu wa Mkoa wa Pwani 

Mbali na hilo Mkuu huyo wa Mkoa amewakumbusha walimu wote ndani ya Mkoa huo kutimiza wajibu wao wa kuelimisha wanafunzi kwani elimu ni muhimu na wao ndio wategemewa wakuu wa uelimisha wa wanafunzi wa ngazi zote.

Naye Ally Hafidhi mmoja wa wazazi amempongeza Mkuu wa Mkoa kwa kuwakumbusha wazazi na walezi wajibu wao kitu ambacho wazazi na walezi wengi wamekuwa wakiwaachia walimu tu kufanya majibu hayo.

Aidha aliongeza kuwa kweli wazazi tumekuwa wazembe kuwauliza watoto wetu kile walichokipata mashuleni kwa siku hiyo kutoka kwa walimu wao.

Kwa upande wake Abiba Mitandi(49) alisema kuwa wazazi walio wengi wanajua jukumu la mzazi ni kuhakikisha mwanafunzi anaendha shule tu lakini la kujua kasoma nini ni suala ambalo linafanywa na walimu tu huko shuleni, sie kama wazazi au walezi kila mmoja kwa nafasi yake anapaswa kujua mwanae kajifunza kipi huko shuleni na hii ikifanyika sawasawa majumbani kwetun itaongeza tija kubwa sana katika Mkoa wetu.

Aidha amemsifu Mkuu wa Mkoa kwa maono yake ya mbali juu ya maendeleo ya Mkoa wetu wa Pwani.

MWISHO

 

 

 

Post a Comment

0 Comments